in

Yanga yapoteza rufani…..

Matumaini ya Yanga kutetea ubingwa wao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara yalipata pigo la kubwa jana wakati Kamati ya Nidhamu ya shirikisho la soka nchini (TFF) ilipotupilia mbali rufaa yao ya kupinga kukatwa pointi 3 walizopata katika mechi dhidi ya Coastal Union baada kumchezesha beki wao Nadir Haroub ‘Cannavaro’ ambaye alipaswa kutumikia adhabu ya kutocheza mechi tatu kutokana na kadi nyekundu aliyopewa katika mechi yao Machi 10 dhidi ya Azam FC lakini akatumikia mechi mbili.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani kutoka katika kikao cha Kamati ya Nidhamu kilicho chini ya mwenyekiti wake Alfred Tibaigana kilichomalizika takriban saa 4 usiku jana, Yanga hawakuwa na hoja za msingi katika rufaa yao na kwamba maamuzi ya mechi ya dhidi ya Azam yalikuwa sahihi.

Kwa maana hiyo, Coastal Union itabaki na pointi tatu na magoli matatu waliyopewa na Kamati ya Ligi kufuatia kosa la Yanga kumchezesha beki huyo wa kati.

Hata hivyo, Yanga bado wanayo nafasi ya kukata rufaa katika ngazi ya juu zaidi ambayo ni Kamati ya Rufaa ya TFF, taarifa hiyo ilisema.

Yanga walikatwa pointi tatu baada ya kushinda 1-0 dhidi ya Coastal Union mkoani Tanga kupitia kwa goli la Hamis Kiiza lakini adhabu hiyo inamaanisha kwamba timu hiyo ya Jangwani itabaki na ponti 43, kumi nyuma ya vinara na mahasimu wao Simba huku zikiwa zimebaki mechi 3 ligi kumalizika.

Yanga imebakisha mechi nne. Azam ni ya pili katika msimamo ikiwa na pointi 50.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Alikhan Popat and John Olaleye in Dar..

Poor infrastructure accounts for tennis players…..