in , ,

Yanga wavunja mwiko Mbeya City


*Wawa wa kwanza kuwafunga Ligi Kuu
*Mwanasoka Omar Changa afariki dunia

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania, Yanga ya Dar es Salaam wameweka rekodi kwa kuwa wa kwanza kuwafunga Mbeya City katika michuano hiyo.

Mbeya City wanaofundiswa na kocha Juma Mwambusi walimaliza awamu ya kwanza ya ligi hiyo kwa ama kushinda au kutoa suluhu na sare mechi zote.

Waliwahi Dar es Salaam mapema baada ya kwenda sare mkoani Pwani kabla ya kukumbana na Yanga ambao pia walikuwa wametoka suluhu na Coastal Union ya Tanga Jumatano.

Hata hivyo, Yanga ndio waliocheka zaidi baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 lililowekwa kimiani na Mrisho Ngasa katika dakika ya 16.

Kocha Mwambusi alieleza kusikitishwa kwake na matokeo hayo ambayo hata hivyo alisema wanayakubali na kwamba wataeweka jitihada zaidi kwenye mechi zinazofuata.

AZAM WATOA KICHAPO CHA HAJA

Katika mechi nyingine kwenye uwanja wa Azam Complex, Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam, Azam waliwachabanga Kagera Sugar 4-0.

Haikuwa rahisi kuamini matokeo hayo kutokana na uimara uliozoeleka wa Kagera Sugar, lakini ndivyo ilivyotokea na Azam kuendelea kukalia uongozi wa ligi kwa tofauti ya pointi moja dhidi ya Yanga.

Brian Omony alifunga mabao mawili wakati kinda Kevin Sunday na Jabir Aziz walifunga moja moja.

TANZIA: OMAR CHANGA AFARIKI DUNIA

Katika tukio jingine la kusitikisha mchezaji wa Moro United aliyepata pia kuzichezea Yanga na nyinginezo, Omar Changa amefariki dunia.

Maiti ya Changa ilikutwa eneo la Jangwani Darajani na haikujulikana chanzo cha kifo chake.

Viongozi wa Moro United walieleza kwamba walikuwa wakishughulikia maandalizi ya maziko yaliyotarajiwa kufanyika Jumatatu hii. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Arsenal warudi kileleni

Mourinho awavunja Manchester City