in , , ,

Wenger: Barca wanapita

Mimi nasema: washapita..

Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amewapa Barcelona asilimia 95 ya

kufuzu kwa hatua ya robo fainali, baada ya ushindi wao wa 2-0.

Mabingwa hao wa Hispania walipata ushindi huo katika uwanja wa

nyumbani wa Arsenal – Emirates, mabao yakifungwa na Lionell Messi,

moja kwa penati katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL).

Wenger aliwalaumu wachezaji wake kwa kushindwa kumalizia vyema upande

wa ushambuliaji na pia kuzubaa uwanjani katika hatua hiyo ya 16 bora.

Alex Oxlade-Chamberlain na Olivier Giroud walikosa nafasi za kuwapa

Arsenal mabao kabla ya kuadhibiwa na Messi.

“Kuna tatizo katika jinsi tunavyomalizia mipira kwenye fursa

tunazopata; kuna kitu tunakosa pale mbele. Barcelona wameshapita kwa

asilimia 95 lakini tunataka kwenda (Camp Nou) na kucheza. Hatuendi

tukichukulia kwamba tumetoka, tutapambana,” akasema Mfaransa huyo.

Messi amemfunga kipa wa Arsenal, Petr Cech kwa mara ya kwanza, kwani

akiwa Chelsea hakufaulu kufanya hivyo.

Arsenal walipambana ili kujipa matumaini na fursa ya kwenda Barca kwa

marudiano wiki tatu zijazo wakiwa na ahueni, lakini sasa itabidi

kwanza wafunge mabao matatu zaidi ya Barca ili wavuke.

Arsenal walionekana dhaifu kwa Barcelona, japokuwa walifanikiwa

kuwadhibiti hadi dakika ya 71 Messi alipofunga.

Nyota watatu wa Barca; Messi, Neymar na Luis Suarez walionekana

kuwatesa Arsenal na kuwaathiri kisaikolojia kwenye mechi hiyo. Messi

alifunga bao la kwanza baada ya shambulizi la kushitukiza, na la

penati lilitokana na kuangushwa na Mathieu Flamini.

Messi sasa ameshawafunga Arsenal mabao manane. Katika mechi hiyo,

Suarez aligonga mwamba wakati Cech alifanikiwa kuokoa mpira hatari wa

Neymar.

Wakitolewa katika hatua hii, itakuwa ni mara ya sita mfululizo. Wenger

amefananisha kipigo hicho na kile cha 3-1 kutoka kwa Monaco msimu

uliopita hatua kama hii hii.

“Nasikitika kwamba kuna wakati tulionekana kwamba tunatawala mchezo,

lakini tukaachia na kuwapa bao, kama ilivyokuwa kwa Monaco msimu

uliopita. Utoto, na hili linachanganya,” akasema Wenger.

Katika mechi nyingine ya UCL, Juventus wakiwa nyumbani walilazimishwa

sare ya 2-2 na Bayern Munich.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

ARSENAL vs BARCELONA JIONI YA LEO…

Tanzania Sports

Fifa mageuzi makubwa