in

Wanariadha wa Kenya wafungiwa kwa madawa

Wakenya wawili wanaoshiriki mbio za marathon wamefungiwa baada ya kutiwa hatiani kwa kutumia dawa za kuongeza nguvu michezoni.

Hatua hiyo inakuja baada ya wanariadha wengine watatu wa nchi hiyo kusimamishwa mwezi uliopita.

Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha cha Kenya, David Okeyo amewataja waliofungiwa kwa miaka miwili ni Salome Jerono Biwott na Jynocel Basweti Onyancha.

Mwezi uliopita, wakimbiaji wa mbio ndefu, Wilson Erupe Loyanae na Nixon Kiplagat Cherutich walifungiwa kwa miaka miwili wakatiMoses Kiptoo Kurgat alipewa kifungo cha mwaka mmoja.

Wiki iliyopita, mwanahabari wa kujitegemea wa Ujerumani, Hajo Seppelt alibainisha matokeo ya uchunguzi kwamba kuna tatizo kubwa la utumiaji dawa za kuongeza nguvu kwa wanariadha nchini Kenya.

Taarifa hiyo ilitolewa kabla ya kufanyika Michuano ya 30 ya Olimpiki jijini London mwaka jana. Kenya na Ethiopia zimekuwa zikitawala kwenye mbio ndefu

“Idadi ya watumiaji dawa hizi inaongezeka na kwa kweli tumeudhika sana na takwimu na hali hii kwa ujumla.

“Tunachoomba tu ni kwamba wakosaji hao wawe katika ngazi inayoweza kudhibitiwa, isije ikatokea tatizo limesambaa kutuzidi nguvu,” akasema Okeyo.

Katika michuano hiyo ya Olimpiki, Kenya iitwaa jumla ya medali 11, mbili zikiwa za dhahabu, nne za fedha na tano za shaba, lakini zinagawanywa katika michezo mbalimbali, ikiwamo riadha.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Uwanja wa Azam kuwa miongoni mwa viwanja vilivyothibitishwa na FIFA kwa Ubora wake.

Rio Ferdinand amejimaliza