in

Vodacom kudhamini Kombe la Soka la Muungano

KAMPUNI ya Simu za Mkononi Tanzania Vodacom imetoa Shilingi 45 milioni kwa ajili ya udhamini wa Michuano ya Kombe la Muungano itakayoanza kutimua vumbi Aprili 26 katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Zanzibar.

Meneja udhamini wa Vodacom, Emiliani Rwejuna alisema udhamini huo utahusisha pia na vifaa vya michezo, gharama za usafiri kwa wachezaji, posho na gharama za maandalizi na zawadi kwa washindi wa kombe hilo.

Alisema mshindi ataondoka kombe na Sh12milioni wakati mshindi wa pili atazawadiwa atazawadiwa kombe na Sh1milioni na wakati mchezaji bora wa michuano hiyo atapata 300,000.

Alisema kwa kawaida mashindano hayo huwa yanaanza katikati ya Aprili na kufikia mwisho Aprili 26 ambayo ni siku ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar lakini mwaka huu yataanza Aprili 26 na kumalizika katikati ya Mei.

Alisema mashindano hayo hujumuhisha timu kutoka Tanzania bara na visiwani na timu hushindana kwa mtindo wa ligi na mwaka huu ztimu zimegawanywa katika vituo viwili bara na kimoja visiwani.

Rwejuna alisema kwa kituo cha Mbeya kitakuwa na timu za Mikoa ya Mbeya, Rukwa na Ruvuma wakati kituo cha mafinga kitakuwa na timu za mkoa wa Iringa na Zanzibar kitakuwa na timu za Zanzibar.

Alisema ilikumpata bingwa mshindi wa mkoa wa Mbeya atacheza na mshindi wa mkoa wa Mfindi na mchezo ni nyumbani na ugenini na mshindi wa hapo atacheza fainali na wa Zanzibar na utakuwa ni nyumbani na ugenini.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply
  1. Hi, I think we should spread this website all over Tanzania so that we can have more views from the Tanzanian because I dont think if all tanzanian they know about it. It is very good website and if we will use it we will do better on Sports as you can see now we have a Good President who is interested on Sports (ila football tu!!!!). he really likes to improve sports in our country basi tu wanam-boa hawa mafisadi na mambo ya kina epa na chenge but he is good.

    Wazo langu: Its better to put this website at the back of each Tanzanian newspaper even if its in small fonts am sure tanzanian will go thru it and discuss on sports issues. It will not cost much. Bwana Saria please try to do this.

    Wish you all the best and many congrats on your good job.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Premier League – Chelsea stay in the race

Premier League – Rampant Arsenal crush Derby