in , , , ,

VAR ina maswali kuliko majibu

Paulo Gazzaniga’s tackle was wild against Chelsea and was rightly called a penalty against Tottenham

Tangu kuanzishwa kwa mfumo mpya wa Mwamuzi Msaidizi kupitia Video (VAR), maswali na changamoto yamekuwa mengi kuliko majibu na suluhisho.

Pamekuwapo migongano mingi juu ya matumizi ya VAR, kwa sababu utata umekuwa mwingi juu ya uamuzi husika, ambapo pia mtiririko wa mechi hukosekana pamwe na ladha yake pale mwamuzi wa kati anapokwenda kuwasiliana na VAR.

Pamoja na makosa yaliyokuwapo uwanjani kwa waamuzi, iwe wa kati au wasaidizi wake washika vibendera sasa wachezaji, makocha, washabiki na wadau wengine wanaonekana kukerwa zaidi na VAR.

Mabao yamekataliwa ambayo kwa mitazamo ya wengi yalionekana ni halali na mmoja wa walalamikaji ni Kocha wa Chelsea, Frank Lampard pamoja na wengine na sasa kocha wa zamani ambaye ni ofisa wa Shirikisho la Soka la KImataifa (Fifa), Arsene Wenger, naye ameona kuna walakini.

Baadhi ya matokeo yaliotokana na VAR
Baadhi ya matokeo yaliotokana na VAR

Anasema kwamba hakuna sababu pale mshambuliaji wa mwisho anapofanya kazi yake, kisha akamzidi beki kwa kiungo kwa kiasi kidogo tu, basi anachukuliwa ameotea. Nakumbuka mchezaji wa Liverpool, Roberto Firmino alipatwa na VAR kuwa ameotea kwa sababu tu bega lake kimahesabu lilizidi lile la mlinzi wa Aston Villa.
VAR inaharibu mtiririko wa mechi na hivyo utamu unaoambatana nao, mbaya zaidi ni pale uamuzi unapokuwa mbaya usioendana na ukweli wa mambo yaliyotokea uwanjani. Uamuzi unaotolewa na VAR mara nyingi umekuwa ukiacha watu wa mpira katika wakati mgumu, ambapo hata wale wanaokuwa wamependelewa hujihisi kwamba haki haikutendeka.

Kwenye mechi baina ya Manchester City na Sheffield United kwenye Uwanja wa Etihad nako kulikuwa na mambo; malalamiko yakawa makubwa dhidi ya VAR lakini hayakusikilizwa; yaliangukia kwenye uziwi.

Sheffield United au Blades kama wanavyojulikana, walishatia mpira kimiani kupitia kwa Lys Mousset lakini VAR ikakataa kwa maelezo kwamba mfungaji alikuwa ameotea.

Baadhi ya matokeo yaliotokana na VAR
Baadhi ya matokeo yaliotokana na VAR

Lakini pia jamaa hao walilalamikia bao la kuongoza la Aguero, kwa sababu mwamuzi Chris Kavanagh alionekana kumzinga na kumzuia John Fleck wakati wa majenzi ya bao hilo. Chris Wilder akaondoka akiwa ameshaungana na waamuzi wanaolia dhidi ya VAR kwenye wikiendi nyingine ambayo VAR imezidi kulalamikiwa.

Wilder alikataa kueleza ni kipi alichokuwa akijadiliana na Kavanagh kwenye chumba cha waamuzi baada ya mechi hiyo, lakini kwa ujumla alionekana kusikitishwa sana na waamuzi hao. Alisema alikuwa anajivunia wachezaji wake na timu kwa jinsi walivyojitahidi.

“Ikiwa unapoteza mechi, kuna njia ya kuipoteza. Lakini nimeiona timu yangu na hali ambayo tumekuwa nayo. Je, tulidhani kwamba tungesonga nayo hadi mwisho wa Desemba? Sidhani. Tumeongezeka katika kujiamini na ujasiri. Ni upinde mkubwa wa kujifunza. Hawa jamaa (Manchester City) wana wachezaji mahiri sana. Klabu mbili hizi ni sawa na tofauti ya miaka miwili ya mwanga kwa umbali; hawakuwa hivyo miaka miaka kadhaa iliyopita.

“Klabu moja haikusonga mbele kwa kasi ambayo City walikuwa nayo, lakini sidhani kwamba pale uwanjani pengo lilionekana kubwa kivile kwa mujibu wa ukali wa mchezo. Timu yangu iliamua kujaribu na ndicho kitu cha msingi tulicho nacho,” anasema

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

Ingenoga Morrison kucheza na Balinya na siyo Yikpe

Tanzania Sports

Nani bora kati ya AJIBU na MIQUISSONE