in

Twiga Stars kwenda Zimbabwe kesho

Timu ya soka ya Tanzania, Twiga Stars, inatarajia kuondoka nchini kesho alfajiri kuelekea jijini Harare, Zimbabwe, kwa ajili ya kushiriki mashindano ya Kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara (COSAFA) ambayo yanatarajiwa kuanza kufanyika Jumamosi jijini humo.

Akizungumza jana, Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura, alisema kuwa msafara wa timu hiyo utakuwa na watu 26 ambapo wachezaji ni 19 pamoja na benchi la ufundi linaloongozwa na Kocha mkuu, Charles Boniface anayesaidiwa na Nasra Mohammed, kutoka Zanzibar.

 

Wambura alisema kuwa mkuu wa msafara wa timu hiyo ni Mwenyekiti wa Chama cha Soka cha Wanawake Tanzania (TWFA), Lina Mhando, ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF.

CHANZO: NIPASHE

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Cole launches soccer players talent scouting

Twiga Stars vs Botswana in Harare