in , , ,

Ratiba Ligi Kuu England yatolewa 2015/16

Kipa wa Chelsea, Petr Cech (33) amewapa matumaini mapya Arsenal baada ya kusema kwamba angependa kubaki London.

*Chelsea wanaanzia nyumbani

Msimu mpya wa Ligi Kuu ya England (EPL) utaanza wiki mja mapema kuliko mwaka jana. Utaanza wiki moja na Football League.

Ratiba ya Ligi Kuu ya England imetoka, ambapo mabingwa Chelsea, wanaanza kutetea ubingwa wao kwa kuwakaribisha Swansea.

Hiyo itakuwa wikiendi ya Agosti 8 na 9 mwaka huu, msimu mpya utakapoanza wakati Manchester City waliomaliza pointi nane nyuma ya Chelsea watasafiri hadi kwa West Bromwich Albion.

Mechi kumi za mwanzo wa msimu 2015/16-EPL
Mechi kumi za mwanzo wa msimu 2015/16-EPL

Arsenal waliomaliza katika nafasi ya tatu wataanza na West Ham wakati waliokuwa wa nne, Manchester United watakabiliana na Tottenham Hotspur katika dimba la Old Trafford.

Liverpool wasiojulikana kama bado watakuwa na Raheem Sterling watapepetana na Stoke, huku Newcastle wakitoana jasho na Southampton wakati Leicester watawakaribisha Sunderland.

Vijana waliopanda daraja msimu huu – Bournemouth, Watford na Norwich watakabiliana na Aston Villa, Everton na Crystal Palace kwa mtiririko huo.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

SAKATA LA RUSHWA FIFA:

Usajili na tetesi zake kutoka England: