in , ,

Man City watwaa Kombe la Ligi

 

Manchester City wamejihakikishia hawaondoki patupu msimu huu, baada ya

kutwaa Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One Cup.

Vijana wa Manuel Pellegrini hawakuwa na kazi rahisi ya kumpa kombe

kocha wao kabla ya kumuaga mwishoni mwa msimu, kwani walilazimishwa

sare ya 1-1 na Liverpool kwenye Uwanja wa Taifa wa Wembley.

Ilibidi waingie kwenye changamoto ya mikwaju ya penati, na ni hapo

kocha Pellegrini alipata raha na karata aliyocheza ya kuendelea

kumtumia kipa Willy Cabalero aliyecheza mechi na dakika zote za

michuano hiyo.

Baada ya kuchabangwa 5-1 na Chelsea kwenye mechi ya Kombe la FA

majuzi, washabiki walionelea kwamba kipa huyo wa Argentina mwenye umri

wa miaka 34 angetupwa kando ili kipa namba moja, Joe Hart arejee

kwenye lango.

Hata hivyo, Pellegrini atakayempisha Pep Guardiola kiangazi kijacho

hapo Anfield, alisema kwamba kuliko amwache Cabalero afadhali

wasilipate kombe hilo, na Jumapili hii alibaki na kipa wake huyo,

kisha baada ya mechi akasema yeye ni mtu wa kusimamia maneno yake.

Caballero alikuwa kipa kwenye kikosi cha Malaga ya Hispania

kilichokuwa kikifundishwa na Pellegrini, kisha alipoajiriwa kuwafunza

Man City akaamua kumsajili. Hata hivyo, hajafanya vyema sana kwenye

mechi za EPL, na Hart amekuwa ndilo chaguo la kwanza mara nyingi.

Wakati Hart akiwa benchi, Cabalero aliokoa penati tatu, ambapo City

walishindwa kwa penati 3-1. Caballero aliokoa penati za Lucas,

Philippe Coutinho na Adam Lallana . katika muda wa kawaida,

Fernandinho alifunga kwa upande wa City muda mfupi baada ya mapumziko

lakini makosa ya mshambuliaji wa zamani wa Liverpool, Raheem Sterling

yaliwazawadia bao Liver kupitia kwa Coutinho aliyesawazisha dakika ya

83.

Katika penati, Fernandinho aligonga mwamba kwa mkwaju wa kwanza wa

City, wakati penati za Jesus Navas, Sergio Aguero na Yaya Toure

zilizama nyavuni. Pamoja na kwamba anatemwa na ‘The Citizens’, tangu

aingie Etihad 2013, Pellegrini amewapatia makombe matatu.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

Arsenal wapotea njia

Tanzania Sports

Leicester wazuiwa lakini …