in , , , ,

Liverpool waponea kwa Rovers

Liverpool wamefanikiwa kuingia nusu fainali ya Kombe la FA baada ya kuwafunga Blackburn Rovers 1-0.

Wakiwa wametoka kupigwa 4-1 na Arsenal kwenye Ligi Kuu wikiendi iliyopita na kufifia matumaini ya kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao, Liver walipata bao kupitia kwa Philippe Coutinho.

Mchezaji huyo wa Brazil alifunga pia kwenye mechi ya marudiano na Bolton katika raundi ya nne na sasa vijana hao wa Brendan Rodgers watachuana na Aston Villa katika Uwanja wa Wembley.

Hata hivyo, bado Liverpool hawakuonesha kiwango kikubwa kwenye mechi ya Jumatano hii, na yaweza kuonekana kwa nini walipoteza mechi zake dhidi ya Manchester United na Arsenal.

Nusu fainali ya kwanza ya FA ni baina ya Reading na Arsenal Aprili 18 na siku inayofuata ndipo Liver watacheza na Villa.

Kipa wa Liverpool, Simon Mignolet aliyeanza msimu chini ya kiwango aliokoa mabao mawili ya wazi kutoka kwa Tom Cairney na Ben Marshall.

Dakika za mwisho alimzuia kipa wa Rovers, Simon Eastwood aliyekaribia kufunga mpira wa kona.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Kitendawili cha Man City na Pellegrini

Gabon mwenyeji AFCON 2017