in , ,

*KIKOSI CHA MOROCCO KUTUA NCHINI IJUMAA*

Timu ya Taifa ya Morocco (Lions of the Atlas) inatarajiwa kuwasili nchini
keshokutwa Ijumaa kwa ndege ya Emirates tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe
la Dunia dhidi ya Tanzania (Taifa Stars) itakayochezwa Jumapili katika
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Msafara wa timu hiyo yenye watu 58 wakiwemo maofisa 19 na waandishi wa
habari 12 utawasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA)
saa 8.55 mchana na utafikia hoteli ya Kilimanjaro Hyatt Regency.

Siku hiyo Morocco inatarajia kufanya mazoezi jioni kwenye Uwanja wa
Kumbukumbu ya Karume, na Jumamosi itafanya mazoezi yake ya mwisho kwenye
Uwanja wa Taifa kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa saa 9 kamili alasiri.

Wachezaji walioko kwenye kikosi hicho chini ya Kocha Rachid Taoussi ni
Nadir Lamyaghri, Anas Zniti, Yassine Bounou, Younnes Bellakhadar,
Abdellatif Noussair, Abderrahim Achchakir, Zoheir Feddal, Younnes Hammal,
Zakarya Bergdich na Abdeljalil Jbira.

* *

Issam El Adou, Kamel Chafni, Salaheddine Saidi, Mohamed Ali Bamaamar,
Abdelaziz Barrada, Salaheddine Aqqal, Abdessamad El Moubarky, Nordin
Amrabat, Chahir Belghazouani, Abdelilah Hafidi, Youssef Kaddioui, Brahim El
Bahri, Hamza Abourazzouk na Youssef El Arabi.

Wakati huo huo, tiketi kwa ajili ya mechi hiyo zitaanza kuuzwa keshokutwa
katika vituo vya Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo,
mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha
Mafuta Buguruni, Uwanja wa Taifa na Dar Live Mbagala.

Milango siku ya mechi kwa ajili ya watazamaji itafunguliwa saa 6 kamili
mchana.

20130320-082134.jpg

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Vikosi vya Yanga na Simba Vilivyotengenezwa Kisayansi (2)

*SERIKALI YARIDHIA MCHAKATO WA UCHAGUZI TFF*