in , , ,

Hapatoshi Man City, United, Chelsea

 

Homa ya nani atakuwa kocha Manchester United kuanzia kiangazi kijacho

imeanza kupanda, huku kocha wa zamani wa Chelsea, Jose Mourinho

akipewa nafasi kubwa miongoni mwa washabiki.

Habari zinasema kwamba ameshaanza mazungumzo na Mashetani Wekundu kwa

ajili ya kuchukua mikoba ya Louis Van Gaal ambaye ameshikilia msimamo

wa kuendelea na kazi hadi mkataba wake umalizike.

Homa nyingine ni juu ya nani atachukua mikoba ya Guus Hiddink ambaye

ni wa mpito Chelsea, aliyeingia kwa ajili ya kufanya ‘ukarabati’ baada

ya Mourinho kuanza vibaya msimu na kuingia Desemba akiwa hoi na vijana

wake.

Joto linapanda zaidi kutokana na ukweli kwamba Manchester City

wameamua kuachana na Manuel Pellegrini mwisho wa msimu na kumtangaza

mapema kocha wa Bayern Munich, Pep Guardiola kwamba atawanoa vijana

wao.

Hali hiyo inawafanya Manchester United kufikiria mara mbili,

ikizingatiwa kwamba katika uongozi na wakongwe wa klabu kulipata

kuwapo mgawanyiko iwapo Mourinho apewe nafasi hapo, wakiona kwamba

atabadili chapa ya klabu na mtindo wa timu.

Tangu kuondoka kwa Sir Alex Ferguson bado Old Trafford hapajatulia,

baada ya Ryan Giggs kupewa mikoba kwa muda kisha akaingia David Moyes

aliyeshindwa au kutopewa nafasi ya kufanya vyema, ama na wachezaji au

na uongozi akafukuzwa.

Van Gaal amekuwa anakosa uendelevu ambapo pia mtindo wake wa soka

hauwapendezi Old Trafford, kiasi kwamba hata wachezaji waandamizi

wamepata kumvaa na kumtaka abadili mfumo, ili wacheze soka ya

kushambulia.

Wakati City wameshatulizana, wakimpata mmoja wa makocha bora na

wanaosakwa zaidi duniani, United na Chelsea bado wamebaki na alama za

kuuliza, huku Arsenal wakiwa hawatarajii jipya zaidi ya kuendelea na

mkongwe Arsene Wenger.

Habari za sasa ni kwamba kuna mwelekeo wa Mourinho kupewa nafasi

United, kwa maelezo kwamba ndiye mwenyewe uwezo wa kukabiliana na

mbinu za Guardiola na hata kukifunga kikosi chake, kama alivyopata

kufanya enzi za The Specia One akiwa Real Madrid na Inter Milan.

Tetesi zinakwenda mbali zaidi sasa na kutaja hata mshahara, zikieleza

kwamba Mreno huyo atalipwa pauni milioni 15 kwa msimu, zikiwa ni pauni

milioni sita pungufu ya Guardiola. Mourinho, 53, inaelezwa kwamba

atamwagiwa fedha hadi pauni milioni 300 kwa ajili ya usajili.

Wasivyokuwa na dogo, wachunguzi wanasema kwamba tayari Mourinho

amemwambia Makamu Mwenyekiti Mtendaji wa United, Ed Woodward kwamba

anataka kuwauza viungo Juan Mata, 27 na Marouane Fellaini, 28.

Ikumbukwe kwamba Mourinho ndiye alimweka kando Mata akiwa Chelsea

kisha kumuuza United.

Mgawanyiko upo bado United, na kuna madai kwamba kocha msaidizi Giggs

ataondoka ikiwa Mourinho atapewa nafasi hiyo, akiamini kwamba ama

wangepaswa kuendelea na Van Gaal wakati yeye akijifunza zaidi au apewe

timu mwenyewe Giggs. Zipo habari pia kwamba, Mourinho yupo tayari

kufanya kazi nje ya Ligi Kuu.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

PSPF yazidi kuvuna wanachama wapya vyuoni

Tanzania Sports

SIMBA YAPAA KILELENI