Ligi Kuu ya England (EPL) imefika patamu baada ya matokeo tofauti

mwishoni mwa wiki.

Wakati vinara Leicester wakienda vyema kwa kuendelea kushinda dhidi ya waliokuwa nafasi ya pili, Manchester City, Arsenal nao wamefufuka.

Baada ya mechi 25, Leicester wapo kileleni na pointi zao 53 wakati

City wakishushwa hadi nafasi ya nne, Arsenal wakipanda had ya tatu

wakifungana pointi na Tottenham Hotspur wanaoshika nafasi ya pili,

wote wakiwa nazo 48.

 

City wanazo pointi 47 wakiwa na kocha Manuel

Pellegrini anayeondoka mwisho wa msimu kumpisha Pep Guardiola aliye Bayern Munich kwa sasa.

Msimamo wa EPL, kwa baadhi ya timu
Msimamo wa EPL, kwa baadhi ya timu

 

Manchester United walipoteza pointi mbili dakika za mwisho Jumapili

hii baada ya kwenda sare 1-1 na Chelsea kwa bao la dakika ya mwisho la Diego Costa, akifuta lile la Man U la Jesse Lingard.

 

Arsenal wao walifunga mabao mawili katika sekunde 88 ugenini

walikokuwa wanacheza dhidi ya Bournemouth kwa mabao ya Mesut Ozil na Alex Oxlade-Chamberlain.

 

Arsenal wamepata ahueni kwani hawakuwa wameshinda tangu Januari 3,

ambapo Jumapili hii Aaron Ramsey alikuwa mchezaji bora wa mechi.

 

Chelsea kwa upande wao walifanikiwa kumpa raha kocha wao wa mpito, Guus Hiddink kwani tangu ajiunge nao hawajapoteza mechi, wamekuwa ama wakishinda au kwenda sare.

Matokeo mengine mwishoni mwa wiki ni kwa Villa kuwafunga Norwich 2-0,

Liverpool wakatoshana nguvu na Sunderland kwa 2-2, Newcastle

wakawabomoa West Bromwich Albion 1-0.

 

Stoke wakiwa nyumbani walilala 0-3 mbele ya Everton, Swansea na

Crystal Palace wakaenda 1-1, Spurs wakawafunga Watford 1-0 na

Southampton wakawashinda West Ham 1-0.

Bado Aston Villa wapo katika hali mbaya, wakishika nafasi ya mwisho

kwenye msimamo wa ligi kwa pointi zao 16, Sunderland wanazo 20,

Norwich 23 na Newcastle 24.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

KONGO DRC YATWAA UBINGWA CHAN KWA MARA YA PILI

Tanzania Sports

PSPF yazidi kuvuna wanachama wapya vyuoni