in , , ,

Daktari Bayern Munich aangushiwa jumba bovu

Kichapo walichopata Bayern Munich cha mabao 3-1 kutoka kwa Porto kimesababisha daktari wa timu hiyo, Hans-Wilhelm Mueller-Wohlfahrt kuachia ngazi.

imageBayern waliochapwa ugenini kwenye mechi ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL) Jumatano hii wanadaiwa kumwangushia jumba bovu daktari huyo, kwa maana kwamba yeye na wasaidizi wake ndio chanzo cha kufungwa kwao.

Mueller-Wohlfahrt (72) ambaye pia ni daktari wa timu ya taifa ya Ujerumani amesema ameshangazwa na kisingizio hicho cha ajabu, na kwamba uaminifu alioujenga katika kazi hiyo na kushirikiana vyema na idara nyingine umeharibiwa.

 

Daktari huyo amefanya kazi na mabingwa hao wa Ujerumani tangu 1977, hivyo uamuzi aliochukua ni mgumu na utawatia simanzi viongozi wa klabu kwa mtu aliyekuwa kama baba hapo.

“Idara yangu imelaumiwa msingi wa timu kufungwa, zikitolewa sababu za ajabu kabisa,” akasema daktari huyo mkongwe aliyepata kuondoka klabuni hapo kwa muda mfupi alipokosana na kocha wa enzi hizo, Jurgen Klinsman.

Katika mechi hiyo, Bayern walicheza bila wachezaji muhimu — Bastian Schweinsteiger, Arjen Robben, Franck Ribery na David Alaba waliokuwa majeruhi, lakini haieleweki ni kwa kiasi gani Mueller-Wohlfahrt ana makosa haijaeleweka.

Kuna video iliyomwonesha Kocha wa Bayern, Pep Guardiola akionesha kumkasirikia mtu kwenye benchi, anayedhaniwa kuwa kocha huyo, baada ya Medhi Benatia kuumia wakati wa mechi dhidi ya Bayer Leverkusen.

Bayern walipoteza mechi kwa idadi ya mabao sawa na Paris Saint-Germain (PSG) waliochapwa na Barcelona.

Hata hivyo, pengine kwa utani, Kocha Guardiola amenukuliwa akisema kwamba pamoja na kusikitishwa na kichapo walichopata, yeye bado ni mtu mwenye furaha. Hakufafanua maneno hayo na huenda ndiye amechangia daktari kufikia uamuzi wa kuachia ngazi.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Klopp atangaza kuachia ngazi Dortmund

Man U, Arsenal wamtaka Higuain