in , , ,

Chelsea, Man City hakuna mbabe

Vinara wa Ligi Kuu ya England (EPL), Chelsea wamekwenda sare ya 1-1 na mabingwa watetezi, Manchester City na kubakisha pengo la pointi tano baina yao
City walitawala mchezo kwa asilimia 57 lakini walitangulia kufungwa kwa bao la Loic Remy dakika ya 41 kabla ya David Silva kusawazisha dakika nne tu baadaye.

Chelsea walicheza bila wachezaji wao Diego Costa aliyefungiwa na Cesc Fabregas aliye majeruhi, huku City wakikosa huduma za wachezaji wa Ivory Coast, Yaya Toure na Wilfried Bony walio Guinea ya Ikweta kwa mechi za Kombe la Mataifa ya Afrika.

Kipa wa Chelsea, Thibaut Courtois alionekana kufanya makosa na wa kulaumiwa kwa bao la City ambao walimchezesha mchezaji wa zamani wa Chelsea, Frank Lamparad katika dakika 17 za mwisho, ambapo washabiki walimpokea kwa kumshangilia.

Jose Mourinho alimtoa mfungaji Remy na nafasi yake kuchukuliwa na beki Gary Cahill akionesha kwamba alikuwa na lengo la kuhakikisha wanalinda sare hiyo na si kuongeza mabao. Manuel Pellegrini wa City hakufurahishwa na kuambulia pointi moja.

Baada ya mechi hiyo, kocha Mourinho hakutekeleza majukumu ya kuzungumza na wanahabari na Ijumaa pia alifuta mkutano wake na wana habari kabla ya mechi hiyo. Kocha msaidizi Steve Holland naye hakuzungumza na wana habari badala yake Remy na Nemanja Matic walizungumza nao.

Katika mechi nyingine, Manchester United walipata ushindi wa pili mfululizo kwenye ligi baada ya kuwakandika Leicester 3-1, yakiwamo mabao mawili ya Robin van Persie na Radamel Falcao huku jingine Leicester wakijifunga kupitia kwa Morgan.

Liverpool walipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya West Ham, ambapo Daniel Sturidge aliyerejea baada ya kuwa amjeruhi kwa muda mrefu alifunga moja, jingine likitiwa kimiani na Raheem Sterling.
Tottenham Hotspur waliwafunga West Bromwich Albion 3-0, Hull wakalala 3-0 pia kwa Newcastle, Crystal Palace wakapoteza 1-0 mikononi mwa Everton, Stoke wakawapiga QPR 3-1 na Sunderland wakawazidi Burnley 2-0.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Guinea Bissau wavuka AFCON

Guinea ya Ikweta, Kongo Kinshasa nusu fainali