in , , , ,

   Arsenal mabingwa FA

 
Hatimaye Arsenal wamemaliza kiu ya taji baada ya kutwaa ubingwa wa Kombe la FA.
Aaron Ramsey ambaye alikuwa tegemeo kubwa kwenye msimu katika ligi kuu ndiye aliwang’arisha Arsenal kwa bao la dakika ya 109.

Arsenal waliokuwa wakipewa nafasi kubwa ya kutwaa taji hilo walikjikuta wakiachwa nyuma kwa kufungwa mabao mapema dakika ya nne na ya nane kabla ya kukomboa dakika za 17 na 71.

Ilikuwa shamrashamra ya aina yake kwenye Uwanja wa Wembley na miaka tisa iliyopita Arsenal walitwaa kombe hili mikononi mwa Manchester United katika Uwanja wa Cardiff.

Wenger sasa anaweza kuanza maandalizi ya msimu mpya ujao vizuri kwa kuwa na kikombe, maana alishasema kuwa hata angekikosa angebaki kuwa kocha wa Washika Bunduki wa London.
 

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Safari ya Taifa Stars kuanza kesho…

Arsenal FA Cup Winners Parade 2014