Leo ilikuwa kama unamsukuma mlevi, ambapo mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania , Yanga, waliwakandamiza JKT Ruvu kwa mabao 5-1.

Wakicheza tena na kipa wao namba moja, Deogratius Munish baada ya Juma Kaseja kucheza mechi ambazo Dida alikuwa ameumia.

Walikuwa na wakati mzuri tangu mechi kuanza, ambapo kama kuna siku Mrisho Ngasa alicheza vyema ni Jumapili hii, ambapo alifunga hat-trick pia Munishi alikuwa mzuri mno langoni.

Mabao mengine yalifungwa na Didier Kavumbagu na Hussein Javu katika mechi ambayo Yanga walicheza kwa kujidai na kujimegea nafasi nyingi za kuatisha vijana wa kocha wao msaidizi wa zamani, Freddy Felix Kataraiya Majeshi Minziro aliyefarijiwa na bao la Nashon Naftali dakika saba kabla ya mpira kumalizika.

Yanga sasa watajiuliza kwa mechi zijazo, kwa sababu wamefikisha pointi 49 wakati Azam wanazo 53 wakiwa wamecheza mechi sawa. Mbeya City wana pointi 46 wakishika nafasi ya tatu.

Yanga wanatakiwa kuwaombea Azam matatizo kwenye mechi zilizobaki, nao washinde, au pia wafanikiwe kwenye rufaa yao dhidi ya Mgambo JKT.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Ubingwa Man City, Liverpool?

Hatimaye Tanzania yaweka rekodi mpya Yalinyakua Kombe la Dunia Kwa Watoto wa Mitaani 2014 Rio de Janeiro