in , ,

Van Gaal astaafu

Kocha wa zamani wa Manchester United, Barcelona na Timu ya Taifa ya
Uholanzi, Louis van Gaal amestaafu.

Van Gaal aliyechukua mikoba ya David Moyes baada ya kustaafu kwa Sir
Alex Ferguson hapo Old Trafford kisha akafukuzwa kazi, amemaliza
kipindi cha miaka 26 ya kufundisha soka.

Van Gaal (65) amekuwa bila kibarua tangu alipofutwa kazi na United Mei
2016, anasema aliwaza kwenda likizo lakini ameona bora aondoke kimoja.
“Nilifikiria huenda ningeachana na kazi hii, ila baadaye nikaona
niende likizo, bali sasa naona nipumzike moja kwa moja na sitarudi
tena kwenye soka,” Van Gaal amekaririwa na gazeti la Kidachi la De
Telegraaf akisema.

Mdachi huyo amepata pia kufundisha klabu za Ajax, Bayern Munich na AZ.
Serikali ya Uholanzi imempa tuzo ya heshima kwa mafanikio aliyolipatia
taifa hilo na yeye mwenyewe kwenye soka.

Akiwa na Man U alitwaa ubingwa wa Kombe la FA msimu wa 2015/16, lakini
akafukuzwa kazi muda mfupi baada ya hapo. Anasema moja ya sababu za
kuachana na soka ni kifo cha ghafla cha mume wa binti yake.

Anasema amekataa ofa nzuri za kufundisha soka Mashariki ya Mbali,
akitaka zaidi kukaa na familia yake. Enzi zake alicheza nafasi ya
kiungo kwa klabu za Ajax, Royal Antwerp, Telstar, Sparta Rotterdam na
AZ kati ya 1972 na 1987 kabla ya kuingia kwenye ukocha.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

AFCON 2017: SARE ZATAWALA MICHEZO YA UFUNGUZI

YEYE ALIMPIGA KOFI MWINYI, MIMI NITAMKARIBISHA KIKOMBE CHA KAHAWA MAGUFULI.