in ,

Ulaya: Vita ya Real na Atletico Madrid

Jumamosi hii ni siku kubwa katika soka kwani miamba wa Hispania, Real Madrid na Atletico Madrid wanavaana kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL).

Ni historia ya aina yake, kwani zinakutana timu kutoka jiji moja. Atletico wanaingia kwenye hatua muhimu baada ya kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Hispania, ikiziacha Barcelona na Real chini yao.

Wakati Diego Simeone akijaribu kukuza wasifu wake zaidi baada ya kuwabomoa Chelsea kwao katika hatua ya nusu fainali. Kwa upande mwingine, Carlo Ancelloti atataka kulinda heshima yake na Los Blancos kwa kuwavisha taji la Ulaya ambalo miaka iliyopita halikuwapa shida kulitwaa.

Atletico watakuwa na hofu kama watakuwa na Diego Costa aliyewasaidia upachikaji mabao, kwani ametokea kuwa majeruhi mara kwa mara.

Hata hivyo wanaweza bado kujidai kwani walipowaaibisha Barca na kutwaa ubingwa wa La Liga hawakuwa naye; aliumia awali. Real wanatamba kwa nyota wao, Cristiano Ronaldo, Gareth Bale walio ghali kuliko timu nzima ya Atletico na wachezaji wengine wengi wazoefu kimataifa.

Mwaka jana fainali ya UCL ilikuwa ya timu za nchi moja – Bayern Munich na Borussia Dortmund za Ujerumani. Bayern walitwaa kombe kabla ya kuvuliwa ubingwa na Real msimu huu kwenye nusu fainali. Kabla ya kutwaa taji Bayern walifungwa kwa mikwaju ya penati na Chelsea katika fainali iliyofanyika kwenye dimba lao la Allianz Arena, Ujerumani.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Cesc Fabregas ataka kurudi England

UJIO MPYA WA KOCHA MAXIMO BONGO