in , ,

Ujerumani wawapopoa Poland

Euro 2017

Ujerumani wamekwea kwenye uongozi wa Kundi D kwenye mechi za kufuzu kwa fainali za Euro 2016, baada ya kuwafunga Poland 3-1.

Yalikuwa mabao ya Thomas Muller aliyefunga kirahisi kwa mpira wa juu huku shujaa wao aliyewapa bao kwenye fainali za Kombe la Dunia nchini Brazil mwaka jana, Mario Gotze akifunga mawili.

Poland walichomoa moja kupitia kwa Robert Lewandowski, bao lililokuja kabla ya lile la pili la Gotze, lililomwacha kipa wa zamani wa Arsenal, Lukasz Fabianski anayekipiga pia Swansea, akishindwa kuzuia.

Jamhuri ya Ireland, katika kundi hilo hilo, waliwafunga Gibraltar 4-0 huku Scotland wakilala 1-0 kwa Georgia. Katika mechi ya mkondo wa kwanza, Ujerumani walilala kwa jirani zao wa Poland 2-0. Ujerumani, hata hivyo, wanaonekana kushuka kiwango uwanjani wakilinganishwa na walivyokuwa kwenye fainali za Kombe la Dunia.

Katika mechi nyingine, Ireland Kaskazini waliwafunga Visiwa vya Faroe 3-1, Finland wakawashinda Ugiriki 1-0, Hungary na Romania wakaenda suluhu sawa na ilivyokuwa kwa Denmark na Albania, huku Serbia wakiwaua Armenia kwa 2-0.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

STARS V NIGERIA: ADUI SI MUSA PEKE YAKE

Tanzania Sports

STARS YASHINDWA KUTAMBA NYUMBANI