in , , ,

Ubelgiji, Argentina robo fainali

Ubelgiji na Argentina wamekata tiketi ya kuingia robo fainali ya michuano ya Kombe la Dunia.

Wakati Ubelgiji waliwafunga Marekani 2-1, Argentina walitokwa jasho kuwashinda Uswisi 1-0, mechi zote zikienda hadi muda wa nyongeza.

Kizazi cha dhahabu cha Ubelgiji kilichanua ikiwa ni mara ya kwanza katika miaka 28 kufika hatua hiyo. Mabao ya Ubelgiji yalifungwa na Kevin de Bruyne na Romelu Lukaku.
Ubelgiji walimwanzisha kinda wao kutoka Kenya, Divoc Origi aliyebadilishwa na Lukaku dakika ya 90 na Origi alikaribia kufunga mara kadhaa. Marekani walipata bao kupitia kwa Julian Green.

Argentina walipata ushindi kwa shida baada ya kubanwa muda mrefu na Uswisi, ambapo Angel Di Maria ndiye alifunga bao pekee la mechi hiyo.

Mabingwa hao wa mara mbili walitawala mchezo lakini ilikuwa vigumu kufanikiwa kucheka na nyavu licha ya kuwa na Lionel Messi.

Argentina sasa watakabiliana na Ubelgiji katika robo fainali Jumamosi hii. Di Maria, hata hivyo, alipoteza nafasi nyingi za kufunga lakini hakukata tamaa.

Argentina waliungwa mkono na washabiki kadiri ya 40,000 kwenye dimba la Arena de Sao Paulo ambapo bao la Di Maria liliwafanya washangilie kwa nguvu kubwa.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

RAGE AMUASA AVEVA

TETESI ZA USAJILI