in

Twiga Stars yatinga nusu fainali COSAFA

Timu ya taifa ya soka ya wanawake, Twiga Stars, imetinga katika hatua ya nusu fainali ya michuano ya Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara (COSAFA), baada ya kuifunga Zambia 2-0 katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Gwanzura hapa Zimbabwe.

 

Kwa ushindi huo, Twiga Stars imefikisha pointi sita baada ya juzi Jumamosi kuwafunga Botswana 3-1.

Twiga sasa itacheza mechi ya mwisho ya hatua ya makundi ya kukamilisha ratiba dhidi ya Afrika Kusini Jumatano.

Katika mechi ya jana, Twiga, ambayo imealikwa katika michuano hiyo baada ya kufanya vyema katika michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wanawake iliyofanyika nchini Afrika Kusini mwaka jana, magoli yote mawili yalifungwa na mshambuliaji Asha Rashid ‘Mwalala’ katika dakika za 21 na 33.

Mechi za hatua ya nusu fainali zitachezwa Alhamisi Julai 7

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Simba cruise into Kagame quarters

Tenga hails Twiga Stars