*Setif na Vita Club zatinga fainali

Klabu yenye washabiki wengi ya TP Mazembe wametupwa nje ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika.
Mazembe wamezidiwa nguvu na Waalgeria wa Entente Setif kwa bao la ugenini.

Katika mechi ya wikiendi hii, Setif walishinda 3-2 katika mechi iliyopigwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Katika mechi ya kwanza nchini Algeria, Mazembe walifungwa 2-1, hivyo mizania inaonesha kwamba wamekwenda 4-4 na Waalgeria wakavuka kwa wingi wa mabao ya ugenini.

Mabao yote ya Setif yalitokana na majalo, yakimwacha hoi kipa mwenye mbwembwe, Robert Kidiaba. Abdelmalek Ziaya alifunga bao zuri katika dakika ya nane tu, wakati Sofiane Younes akitoka benchi alifunga bao kipindi cha pili.

Mazembe walicharuka na kupata mabao kupitia kwa Daniel Adjei, Salif Coulibaly na Joel Merikani
Setif waliwaumiza Mazembe dakika 11 tu kabla ya mechi kumalizika walipofunga bao na kufanya wawe nguvu sawa na kuingia fainali kwa mara ya kwanza tangu 1988 walipofika fainali.

Sasa Setif watakabiliana na Wakongomani wengine, AS Vita Club kwenye fainali, ambapo kama Mazembe wangevuka ingekuwa fainali ya kihistoria kukutanisha timu za taifa hilo.

Vita wameingia fainali baada ya kuwatoa CS Sfaxien wa Tunisia kwa jumla ya mabao 4-2.

AS Vita Club wataanza kuwa wenyeji wa Entente Setif Oktoba 26 kwenye fainali ya kwanza kabla ya kusafiri hadi Algeria Novemba mosi.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Kimetto rekodi mpya Marathon

Chelsea wajidai kileleni