in

TBF Inatafuta wafadhili wa Ujio wa Wamarekani wa Kikapu!!

SHIRIKISHO la Mpira wa Kikapu Tanzania (TBF), linasaka wafadhili wa ziara ya wachezaji wa mpira wa kikapu kutoka vyuo vikuu vya Marekani wanaotarajia kuja nchini kwa ziara ya kimichezo mapema mwezi Juni.

Akizungumza juzi, Rais wa TBF, Richard Kasesela, alisema timu ya Young life kutoka Marekani inatarajia kuja nchini kwa mashindano ya kimataifa na timu za Tanzania.

Alisema timu hiyo inaundwa na wachezaji kutoka vyuo mbalimbali vinavyo shiriki ligi maarufu ya vyuo vya NCAA na kuunda timu ya Young Life America.

Ujio huo wa watu 35, una lengo la kuendeleza kiwango cha mpira wa kikapu nchini, kuendesha mafunzo ya mchezo huo kwa wachezajina makocha.

Pia alisema watakuza uhusiano baina ya vijana wa kitanzania na Marekani na kuhamasisha ujenzi wa viwanja vya mpira wa kikapu katika Manispaa za Dar es Salaam na baadae kuhamasisha mikoani.

Alisema licha ya Dar es Salaam, pia timu hiyo inatarajia kufanya kliniki mkoani Pwani, kwenye kituo cha michezo cha Filbert Bayi na kutembelea Zanzibar kwa mchezo mmoja.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Ghana hope to end decade of disappointment

Boxers get 7m/- shot in the arm