in , , ,

Arsenal kicheko, Man Utd majanga

* Man Utd yapoteza kwa Southampton
*Arsenal yainyanyambua Stoke City

Baada ya kuonekana kama mambo yanataka kutengemaa kwa Manchester United huku wakivuna pointi 37 na kushika nafasi ya tatu baada ya mechi 20, leo mambo yamegeuka na kujikuta wakiruhusu kichapo cha bao 1-0 wakiwa Old Trafford dhidi ya Southampton na kushuka hadi nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi kuu Uingereza.

Bao pekee kutoka kwa kiungo mshambuliaji wa Southampton, Dusan Tadic lililopatikana kipindi cha pili, lilitosha kuwapatia alama tatu muhimu vijana wa kocha Ronald Koeman ambao msimu huu wanaonekana kuwa moto wa kuotea mbali.

Pointi hizo muhimu za leo zimewapeleka hadi kwenye nafasi ya tatu baada ya kutimiza alama 39 kutokana na mechi 21 walizocheza hadi sasa. Tofauti na wengi walivyodhani, Southampton ndiyo timu iliyoruhusu kufungwa mabao machache mpaka sasa kuliko timu yoyote (mabao 15 pekee) licha ya kuuza watu kama Dejan Lovren.

Pamoja na kuonyesha kupambana, Manchester United hawakuweza kulenga hata shuti moja golini na hii ni dalili tosha kuwa safu ya ushambuliaji ya vijana wa kocha Loius Van Gaal hawakuwa katika ubora kwenye mchezo wa leo licha ya kumiliki mpira kwa asilimia 60.

Kwa upande wa pili, leo kulikuwa na mchezo mwingine pale katika dimba la Emirates ambapo Arsenal walikuwa nyumbani kuwaalika Stoke City na mchezo huo umemalizika kwa Arsenal kupata ushindi wa mabao 3-0.

Alexies Sanchez aliendelea kuwa Mfalme wa magoli kwa upande wa Arsenal baada ya kufunga mabao mawili na kufikisha jumla ya mabao 12 ya ligi kuu msimu huu huku lile la tatu, likifungwa na beki wa kati, Laurent Conscienly.

wanyama
Wachezaji wa Southampton wakipongezana baada ya kuangusha “mbuyu”

Huu unakuwa ni ushindi wa 10 wa Arsenal msimu huu na hivyo baada ya kutimiza alama 36, wamepanda hadi kwenye nafasi ya tano na tofauti kati yao na Manchester United walioko kwenye nafasi ya nne, ni alama moja pekee.

Katika mchezo huo, kocha Arsene Wenger alishuhudia mchezaji wake Matthieu Debuchy akitolewa nje kwa Machela baada ya kuteguka bega wakati akigombea mpira na mchezaji wa Stoke City, Marko Arnautovic.

Katika hali ya kawaida wakati kama huu ligi ya EPL hujigawa katika makundi matatu. Chelsea ambao wana alama 49 na Manchester City wenye alama 47, wanaonekana kupewa nafasi kubwa ya mmoja kuibuka na ubingwa na hili ni kundi la kwanza.

Mata alipata nafasi nzuri ya kuweza kuipatia timu yake bao, lakini hakuwa makini langoni.
Mata alipata nafasi nzuri ya kuweza kuipatia timu yake bao, lakini hakuwa makini langoni.

Kundi la pili ni lile linalowajumuisha Manchester United, Liverpool, Arsenal, Tottenham, Southampton na West Ham United ambao wanapigania kumaliza kwenye moja kati ya nafasi nne za juu ili kupata ushiriki wa Michuano ya Uefa msimu ujao.

Na kundi la mwisho, ni wale ambao wanapambana kukwepa kushuka daraja. Katika vita hii unakutana na timu kama Leicester City, Burnley, Crystal Palace, West Brom na hata QPR.

Msisimko kama huu ndiyo unaifanya ligi ya England kutotabirika kwani kila mchezo unakuwa na umuhimu kwa pande zote

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Wilfried Bonny huyoo Man City

AFCON yaja na maswali mengi