in , ,

Uzembe Afrika waisononesha Fifa

 
Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) limesikitishwa na hali ya mataifa kadhaa ya Afrika kutokuwa makini kiasi cha kuchezesha wachezaji wasiotakiwa.

Fifa imesema inasononeshwa na jinsi timu zinavyokiuka kanuni za wachezaji wasiotakiwa kucheza, tena kwenye mechi za kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia 2014.

Mkurugenzi wa Mashindano wa Fifa, Mustapha Fahmy anasema inasikitisha kuona kwamba mechi nane zimebadilishwa matokeo kutokana na moja ya timu kwenye kila mechi kuchezesha mchezaji aliyezuiwa kwa sababu ya kadi nyekundu.

Katika mechi zote, timu pinzani na ile iliyochezesha mchezaji asiyetakiwa ilipewa ushindi wa mabao 3-0 na pointi tatu na kuathiri kwa kiasi kikubwa misimamo kwenye makundi.

Anasema hajui tatizo liko wapi kwani kanuni zipo wazi na kwamba siku zote Fifa wamekuwa wakitoa ushirikiano ili mashindano yote yaende vizuri.

Cape Verde wameathiriwa kwa kiasi kikubwa na tatizo hilo, ambapo licha ya kufanya vyema sana kwa mara ya kwanza kwenye kufuzu huko na kuwashinda Tunisia 2-0 jijini Tunis, waliadhibiwa na kupokonywa mabao na pointi zote na kutupwa nje ya mashindano kwa kuchezesha mchezaji aliyekuwa anatumikia adhabu.

Guinea ya Ikweta nayo ilipoteza pointi tatu kwa sababu hiyo hiyo walipocheza na Cape Verde kabla.
 

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Man United wachanganywa Ukraine

Fifa yaunda Kamati Maalumu ya Qatar