in , , ,

Utata penati ya Messi

*Nyodo na dharau kwa timu pinzani, au ni kujiamini?
Uamuzi wa nyota wa Barcelona kucheza penati kwa mtindo tofauti umezua

utata kwenye ulimwengu wa soka.

 

Wapo wanaodhani kwamba nyota wa Barcelona – Lionel Messi, Luis Suarez

na Neymar walionesha dharau kwa timu pinzani ya Celta Vigo.

Messi ndiye aliyepiga penati, lakini badala ya kupiga moja kwa moja

langoni, akampasia Suarez aliyekuwa nje ya boksi la penati, naye

akautia mpira wavuni.

 

Penati hiyo ilipigwa Barca wakiongoza kwa 3-1 na baadhi, ikiwa ni

pamoja na kocha wa Barcelona, Luis Enrique, wanaona ilikuwa hatari

kwani uwezekano mkubwa ulikuwa kukosa bao.

 

Ni kwa sababu hiyo baadhi ya wachambuzi wanaona kwamba Barca

waliwadharau wapinzani wao, ndiyo maana badala ya kutumia fursa hiyo

ya penati ambayo ni ‘bao kwa zaidi ya asilimia 90’ kuigeuza kama mpira

wa adhabu ndogo.

 

Neymar anadai kwamba walifanya mazoezi kwa ajili hiyo na kwamba mpira

huo ilikuwa apewe yeye, ila Suarez akauchukua kutoka kwa Messi,

akikimbia haraka kutoka nje ya boksi la penati.

 

Kiungo wa Barcelona, Andres Iniesta alisema hawakuwadharau wapinzai

wao, akikiri si kitu cha kawaida kupiga vile lakini akafurahi kwamba

mbinu hiyo ilifanya kazi na hakuna haja ya kuwa na mjadala kwenye

hilo.

 

Katika mechi hiyo Barca walishinda 6-1. Kocha wa Celta Vigo, Eduardo

Berizzo alisema ni njia tofauti ya kupiga penati. Hata hivyo, alidai

wachezaji wa Barcelona hupenda zaidi kujionesha kwa mtindo wanaotumia

kuliko kushinda tu mechi.

 

Enrique, mchezaji wa zamani wa Barcelona, alisema angekuwa yeye

hangecheza vile, kwa sababu angeweza kuukanyaga mpira, kuanguka na

kukosa bao.

 

Wengine wanaona kwamba Messi alikuwa akitoa heshima kwa mkongwe wa

zamani wa Barca, Johan Cruyff aliyefanya hivyo akiwa na Ajax 1982.

Arsenal walijaribu hilo dhidi ya Manchester City 2005, lakini Robert

Pires hakuweza kuupata na kuufunga mpira aliopelekewa na Thierry

Henry.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

Arsenal waangusha mbuyu

Tanzania Sports

Chelsea wapigwa, kocha ajifariji