in

Thabeet awapa vipande vyao akina naniiii!!

NYOTA wa mchezo wa kikapu wa Tanzania, anayecheza katika ligi ya NBA ya Marekani Hasheem Thabeet amesema viongozi wa mchezo huo nchini wasimtumie kama ngazi kwani mafanikio aliyoyapata ni juhudi zake binafsi.

kikwetes

Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi usiku katika hafla iliyoandaliwa na Kaimu Balozi wa Marekani nchini, Larry Andre, Hashim alisema ameshangazwa na viongozi wengi kumtumia yeye kama daraja kwa kujidai kuwa ndio waliomsaidia hadi hapo alipofikia wakati si kweli.

”Nadhani kuna watu wanataka kujinufaisha kwa kusema wamenisaidia kwa ajili ya uchaguzi wa chama chao, lakini si kweli. Nashangaa baadae wengine wamenifuata hadi Marekani na kudai kuwa wametumwa kunipongeza alisema.”

Hashim alikuwa akimaanisha baadhi ya viongozi waliomfuata huko kwa madai wametumwa na Rais Kikwete kwa kuwa amekuwa akimtembelea mara nyingi na kumpa moyo.

Akizungumzia kuhusu mchezo huo nchini, Hashim alisema mpira wa kikapu utachukua miaka mingi kufikia mafanikio kwa kuwa viongozi hawana nia ya kusaidia wachezaji.

”Watu wanaohusika ndio wanafanya mchezo huu ushindwe kuendelea kwani tangu niondoke nchini hadi sasa, hali ni ileile hakuna maendeleo, hata viwanja viko katika hali ileile,” alisema.

Alitahadharisha kuwa kutokana na hali hiyo itakuwa vigumu kwa Mtanzania mwingine kupata nafasi kama yake kwa hapa nchini bila ya kujipeleka mwenyewe kwa juhudi zake, ìlabda mmoja katika milioni moja sijui kama itatokea.”

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Celtic 0 – 2 Arsenal

Premier League – Blake screamer stuns United