in , ,

Serena Williams hana mpinzani

Mcheza tenisi maarufu, Serena Williams ameweka rekodi kwa kufikisha taji la 21 la Grand Slam.

Serena Ametwaa ubingwa wa sita wa Wimbledon na kukamilisha kile kinachoitwa ‘Serena Slam’.

Mmarekani huyu amefikia hatua hiyo baada ya kumshinda Garbine Muguruza wa Hispania na sasa ndiye anashikilia mataji yote manne makubwa duniani.

Serena (33) alishinda kwa seti 6-4 6-4 hivyo kufikisha taji la 21 la Grand Slam, likiwa pia ni taji la tatu kwa mwaka huu pekee.

Alifanikiwa kuzuia makali ya Muguruza (21) aliyejaribu kurejea mchezoni na hatimaye akaibuka kidedea baada ya saa moja na dakika 23.

Baada ya kumaliza kazi hiyo, Serena ataelekea US Open mwezi ujao akidhamiria kukamilisha kalenda ya kwanza ya Grand Slam tangu aanze mchezo huo kiushindani.

Kwa Muguruza ilikuwa mara yake ya kwanza kucheza katika fainali ya Grand Slam na awali aliongoza kwa 4-2 akimtisha vilivyo Serena ambaye alitulia na kuifanya kazi yake sawa sawa.

Serena amekiri kwamba kulikuwa na shinikizo kubwa upande wake, hasa dakika za mwisho, akisema Mhispania huyo alicheza vyema kiasi cha kumfanya afikirie kukwama kutwaa taji hilo.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Schweinsteiger huyoo Man United

MANCHESTER UNITED WAAPA