in , , ,

Arsenal waangusha mbuyu

 

*Man City hali ngumu, Liver waua

Mzunguko wa 26 wa Ligi Kuu ya England (EPL) umekamilika kwa matokeo

mchanganyiko, vinara wa ligi hiyo, Leicester wakipnguzwa nguvu.

Wakicheza ugenini kwa Arsenal, Leicester walikubali kichapo cha 2-1,

lakini ndio walioanza kufumania nyavu.

Danny Welbeck aliyerejea kutoka kwenye majeraha ya muda mrefu ndiye

alikuwa shujaa wa mechi kwa kufunga bao la ushindi sekunde za mwisho

za mechi hiyo.

Welbeck...
Welbeck…

Leicester walibaki wachezaji 10 baada ya kadi ya pili ya njano kwa

Danny Simpson mapema kipindi cha pili, lakini walicheza vyema kwa

kujipanga, chini ya kocha wao, Muitaliano Claudio Ranieri ‘The

Tinkerman’.

Welbeck alikuwa akicheza mechi yake ya kwanza ya kiushindani tangu

Aprili mwaka jana, ambapo aliupokea vyema mkwaju wa adhabu ndogo wa

Mesut Ozil, akafunga baada ya kumzidi maarifa kipa Kasper Schmeichel

na kuamsha ushangiliaji mkubwa Emirates.

Hii ni mechi ya tatu tu kwa Leicester kupoteza. Jamie Vardy ndiye

alifunga bao la kwanza kwa penati baada ya kuonekana kuanguka kutokana

na Nacho Monreal kumnyooshea mguu wake.

Theo Walcott aliingia kipindi cha pili na kufunga bao zuri kutokana na

mpira wa mshambuliaji mwenzake, Olivier Giroud.

Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger alisema kwamba alifurahishwa na

ushindi kwa sababu walishinda jaribio gumu kisaikolojia na sasa wapo

kwenye ushindani wa kutafuta ubingwa wa England, kwani wapo pointi

mbili tu nyuma ya vinara Leicester.

MAN CITY WADUWAZWA NA SPURS

Manchester City, wanapitia kipindi kigumu..
Manchester City, wanapitia kipindi kigumu..

Manchester City wanaomsubiri kocha mpya kiangazi kijacho, Pep

Guardiola wamefanya vibaya kwenye mechi yao, wakipoteza kwa Tottenham

Hotspur.

Spurs sasa wanashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi,

wakifungana pointi na Arsenal, lakini wakiwa na uwiano mzuri zaidi wa

mabao.

Christian Eriksen ndiye alifunga bao dakika za lala salama baada ya

lile la Harry Kane baada ya lile la Kelechi Iheanacho wa Manchester

City.

Huu ni ushindi wa tano mfululizo kwa Spurs, wakionesha kuwa timamu,

kujiamini na moyo wa kupata ushindi chini ya kocha Mauricio

Pochettino.

Manuel Pellegrini alionekana kusikitishwa na vijana wake, kwani tamaa

yake sasa ni kuondoka akiwa amewapa ubingwa kwa mara ya pili. Wamevuna

pointi 26 katika mechi 17 zilizopita, rekodi ambayo bado si nzuri

kulinganisha na ushindani mkubwa uliopo. Wameachwa pointi sita nyuma

ya vinara Leicester wenye pointi 53.

LIVERPOOL WAFANYA MAUAJI

Mashabiki wa Liverpool wakimpongeza ORIGI
Mashabiki wa Liverpool wakimpongeza ORIGI

Liverpool wamefanya mauaji kwa Aston Villa kwa kuwakandika mabao 6-0.

Majeruhi wa muda mrefu aliyerejea dimbani, Daniel Sturridge alifungua

kitabu cha mabao, akicheza mara ya kwanza tangu Oktoba mwaka jana.

Mabao mengine yalifungwa na Emre Can, Divock Origi, Nathaniel Clyne,

Kolo Toure. Hii ni mara ya kwanza tangu 1983 kwa Villa kukubali

kichapo cha mabao sita.

Kwa matokeo ya jumla wikiendi hii, Leicester wanashika nafasi ya

kwanza wakifuatiwa na Spurs, Arsenal na Man City.

Mkiani wapo Aston Villa wenye pointi 16, juu yao wapo Sunderland na

pointi 23, moja zaidi ya Newcastle na Norwich.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

Man U hoi, Chelsea kicheko

Tanzania Sports

Utata penati ya Messi