in , ,

Muhammad Ali hoi kitandani

BINGWA wa zamani wa uzani wa juu wa ngumi duniani, Muhammad Ali yupo taabani kwa ugonjwa kitandani.
Rahman Ali, ambaye ni ndugu yake Muhammad, amesema kwamba kaka yake anaumwa hivyo kwamba amefikia hatua ya kushindwa kuzungumza. Nyota huyo aliyetamba kwa muda mrefu na kupendwa sana, aligundulika kuwa na ugonjwa wa kutetemeka mwaka 1984.

Ali (72) alikuwa mgonjwa hivyo kwamba Jumatano iliyopita alishindwa kwenda Hollywood kwa ajili ya kushuhudia filamu kuhusu maisha yake iitwayo ‘I Am Ali’, ambapo Rahman alikwenda na bintiye Ali. Filamu hiyo itazinduliwa nchini Uingereza Novemba 28.

“Sikuweza hata kuzungumza na kaka yangu (Ali) juu ya filamu hii kwa sababu ni mgonjwa sana na anazungumza kwa shida. Alishatukubalia tuendelee na kazi hii kwa hiyo ni wazi anaona fahari kwa sisi kuwa hapa,” akasema Rahman Jumatano hiyo akiandamana na binti wa Ali, Maryum mwenye umri wa miaka 46.
Rahman ni mdogo kwa Ali kwa mwaka mmoja tu, na amesema kwamba kaka yake amekuwa shupavu kupambana na ugonjwa huo kwa karibu miaka 30 sasa.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Di Matteo kocha mpya Schalke

Valdes awazodoa Liverpool