in ,

Ghana wavuka, ‘vita’ yaibuka uwanjani

Ghana wamekata tiketi kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) katika mazingira magumu, baada ya washabiki wa wenyeji Guinea ya Ikweta kuwashambulia wachezaji na maofisa, kwa madai ya kutoridhishwa na mwamuzi.

Black Stars walishinda 3-0 na kukatisha ndoto za alinacha za wenyeji kufika fainali, baadaya kuwa wametinga nusu fainali kiutata kwa ushindi dhidi ya Tunisia wa 2-1, ambapo mwamuzi aliyechezesha amefungiwa miezi sita.

Vurugu zilianza kwa washabiki kurusha chupa za maji uwanjani, lakini pia vitu kama sahani na mawe viliokotwa dimbani baadaye, ikabidi mchezo usitishwe kwa muda, wachezaji wakingwe kwenda vyumbani na polisi watumie mabomu ya kutoza machozi dhidi ya washabiki wakorofi, huku helikopta ya polisi ikirandaranda juu ya dimba kuhakikisha usalama.

Wachezaji wa Guinea ya Ikweta nao waliathiriwana vurugu hizo mjini Malabo, waliokuwapo wakielezea kwamba ilikuwa kama hali ya kivita, washabiki wa Ghana wakakimbia kujificha nyuma ya lango lao ili kuepuka kupigwa na wale wa wapinzani wao. Mashabiki kadhaa wamedakwa na polisi, na wapo waliomsogelea mwamuzi kumchapa.

mashabiki

Mechi hiyo iliyosimamishwa kwa dakika 30 ilirejea baada ya polisi kufanikiwa kutuliza ghasia na kuimarisha ulinzi kila upande, na sasa Ghana watacheza dhidi ya Ivory Coast katika mechi inayotarajiwa kuwa tamu Jumapili hii. Ivory Coast waliwatoa Kongo Kinshasa kwa mabao 3-1 Jumatano.

Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) lilitumia vipaza sauti kutishia kufutilia mbali mechi hiyo iwapo washabiki wangeendeleza fujo lakini Rais wa Chama cha Soka cha Ghana, Kwesi Nyantakyi baada ya mechi alisema halikuwa tukio kubwa kihivyo, bali palikuwapo njama za kuitia doa Afrika kwa kulikuza.

Mabao ya Ghana yalifungwa na Jordan Ayew katika dakika ya 42 baadaya Kwesi Appiah kuchezewa visivyo na kipa Felipe Ovono. Dakika tatu tu baadaye waliongeza bao la pili kupitia kwa Mubarak Wakaso baada ya shambulizi la kushitukiza.

Ni baada ya mabao hayo na wakati wa mapumziko ndipo washabiki walianza vurugu, pengine wakitaka yatokee ya kwenye mchezo wao na Tunisia uliopita ambapo walipewa penati isiyokuwa halali dakika ya 90 na hatimaye kuja kuibuka na ushindi.

Bao la tatu na lililotia msumari wa mwisho kwenye jeneza la wenyeji lilifungwa na Andre Ayew katika dakika ya 75 na baada ya hapo, washabiki walianza kutafuta pa kujificha.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Kutoka TFF..

KAMATI YA NIDHAMU YAWAADHIBU NYOSO, MORRIS