in , , ,

KUFUZU KWA EURO 2016

Vurugu zavunja mechi ya Urusi

Vurugu kubwa zimejitokeza uwanjani na kusababishwa kuvunjwa kwa mechi ya kufuzu kwa mashindano ya Euro 2016 baina ya Urusi na Montenegro.

Dalili za fujo zilionekana mapema katika Uwanja wa Gradski ulioko Podgorica, kwani katika dakika ya kwanza tu ya mchezo, kipa wa Urusi, Igor Akinfeev alipigwa kwa fashifashi kichwani.

Katika mechi hiyo ya Kundi G, kipa Akinfeev alipigwa nyuma ya kichwa na kulazimika kutolewa nje kwa machela kwenda kupata matibabu na nafasi yake kuchukuliwa na kipa mwingine.
Mechi hiyo ilisimama kwa muda wa dakika 35, ndipo mwamuzi Mjerumani, Deniz Aytekin akauanzisha tena.

Hata hivyo, timu zikiwa bado kufungana, katika nusu ya pili vurugu zilizuka, ambapo wachezaji wa Urusi walipigana na wale wa Montenegro, ambapo watu wa benchi la ufundi nao walihusika.
Katika kipindi cha pili mchezo ulisimama kwa dakika 18 baada ya kuzuka vurugu baada ya penati ya Roman Shirokov ya dakika ya 66 kuokolewa na kipa wa Montenegro, Vukasin Poleksic.

Kutokana na vurugu kuzidi huku kukiwa hakuna dalili za utulivu wala amani, mwamuzi hatimaye aliamua kuvunja mechi hiyo.
Shirikisho la Soka la Ulaya (Uefa) limesema kwamba linasubiri kupata ripoti ya mwamuzi na mjumbe wake kabla ya kuchukua hatua za kinidhamu.

Montenegro ambayo ilimtumia mshambuliaji wa Manchester City, Stevan Jovetic wamefungana na Urusi kwa pointi tano
Inaelezwa kwamba kipa Akinfeev alipelekwa hospitalini kwa matibabu zaidi, ambapo alipata majeraha ya moto na kuumia shingo.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

England wawachakaza Lithuania

Tanzania Sports

Mazungumzo yangu na shabiki wa Arsenal, jijini London.”asenali” Yasin Aden