in , ,

Dnipro, Sevilla fainali Europa

Mabingwa watetezi wa Ligi ya Europa, Sevilla wamefanya vyema kwa kuingia fainali.

Fainali ya Ligi ya Europa itawakutanisha Dnipro na mabingwa watetezi, Sevilla baada ya Dnipro kuwachapa Napoli.

Mshambuliaji wa Ukraine, Yevhen Seleznyov ndiye alifunga bao pekee katika mchezo huo. Fainali itachezwa jijini Warsaw, Poland Mei 27.

Sevilla walio Ligi Kuu ya Hispania walikamilisha kazi yao kwa kuwachapa Fiorentina 2-0 na kuwatoa kwa uwiano wa mabao 5-0.

Kuingia nusu fainali kwa Fiorentina na Napoli kulitoa uwezekano wa timu za Italia kucheza fainali hivyo kujihakikishia kutwaa kombe, lakini walipoteza fursa hizo.

Katika kipindi cha miaka 10 Sevilla wametwaa ubingwa huo mara tatu na sasa wanasaka kuweka rekodi ya kipekee Ulaya kwa kulitwaa mara nne.

Mshindi atafuzu moja kwa moja kwa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL).

UCL ndiyo michuano mikubwa zaidi Ulaya, yenye heshima kubwa na fedha, ambapo timu za ligi mbalimbali hupambana kufuzu.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Bale, Kane watakiwa Man United

Waziri wa michezo Ivory Coast atimuliwa