in

Afrika Kusini kuandaa Kombe Afrika 2013

Shirikisho la Soka Barani Afrika (Caf) limetangaza Afrika Kusini itaandaa mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika ya Soka mwaka 2013 badala ya Libya.

Libya imeichia nafasi ya kuandaa mashindano hayo kutokana na hali kutokuwa shwari nchini humo.

Badala yake Libya itaandaa mashindano ya mwaka 2017, ambayo ilikuwa awali yafanyike nchini Afrika Kusini.

Kubadilishana huko ni makubaliano baina ya nchi hizo mbili ambayo yalifahamika wiki mbili zilizopita.

Wakati huo Caf ilisema tangazo hilo limetolewa mapema mno, huku Nigeria na Algeria pia zilionesha nia ya kuandaa.

Nigeria ilitajwa kuwa nchi itakayosubiri wakati Caf ilipotoa tangazo la awali kuhusu wapi mashindano ya kuuanzia mwaka 2010 – 2014 yatakapofanyika.

Lakini uamuzi wa kufanya mashindano hayo Afrika Kusini, uliidhinishwa na mkutano wa Kamati ya Utendaji ya Caf unaofanyika mjini Cairo.

Afrika Kusini pia itachukua nafasi ya Libya kuandaa michezo ya mwaka 2014 ya Mataifa ya Afrika, kwa wachezaji wanaotimua ligi za nyumbani.

Mapema mwaka huu waliandaa pia mashindano ya vijana ya Afrika chini ya miaka 20, ambayo Libya ilishindwa kuandaa.

Caf pia ilitangaza nchi mbalimbali zitakazoandaa mashindano kadha makubwa.

Namibia itandaa mashindano ya Wanawake ya mwaka 2014 ya Ubingwa wa Afrika na Niger itachukua jukumu la kuandaa mashindano ya mwaka 2015 chini ya umri wa miaka 17 .

Senegal itakuwa mwenyeji wa fainali za mwaka 2015 chini ya umri wa miaka 20, wakati Madagascar itakaribisha nchi nyingine katika kuwania ubingwa wa mashindano ya umri wa chini ya miaka 17 ya mwaka2017.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Tambo za Yanga, Simba katika soka la Tanzania zinakaribia mwisho

Baraza jipya la Michezo la Taifa (BMT)