in

Soka inaanza kuamka

Hali inaonesha kwamba sasa soka inaanza kuamka dhidi ya fedha inayozalisha yenyewe.

Kama usemi wa zamani unavyokwenda, ikiwa unakipenda kitu, basi ukitumikie na kukitunza – na kwa asili, huku ukibaki na umiliki wa yote muhimu, mali pamoja na fedha.

Habari kwamba Roman Abramovich anaachana na shughuli za siku hadi siku katika udhibiti wa Chelsea akiwaachia wadhamini na wakfu yao, zimechukuliwa na kutafsiriwa kwa mapana na kwa njia tofauti.

Kwa baadhi, kuchukua hatua hiyo ni sawa na sadaka au aina ya ibada: jinsi alivyokuwa akiilinda klabu aliyoipenda dhidi ya matishio mbalimbali, ukosoaji au hata kunyakuliwa. Hatua hii imekuja kwa kushangaza juu ya bilionea huyu.

Kwa wengine, uamuzi wake wa kujing’atua na kukaa kando ni jambo la kawaida au hata kukwepa majukumu yake hapo, akiwa ametoa kauli sahihi isiyokuwa na ingizo la kisheria kwa namna yoyote.

Kwa baadhi ni kwamba hizi ni dalili kwamba mambo hayatakuwa tena kama kawaida, japokuwa kwa wengine hii ni ishara kwamba Abramovich anayo nia ya kuhakikisha kila kitu kinabaki kuwa cha kawaida.

Uhakika ni kwamba iwapo Abramovich alikuwa na nia ya kufafanua juu ya hali ya umiliki, au ikiwa alidhamiria kuiuza Chelsea au kipi kinachomaanishwa na ‘utumishi na kujali’ au idadi ya mambo kwa sasa yanayowatia wasiwasi washabiki wa Chelsea, basi angekuwa ametoa ufafanuzi huo.

Ingekuwa vyema zaidi iwapo tungemuuliza, sivyo? Tenga muda, kaa naye kitako kwa saa moja na waandishi wa chache au hadhira ya washabiki wa Chelsea. Chota akili zake, fyatua maswali ya kutosha.

Lakini kwa kuwa hali hii imebakisha sintofahamu, ikibaki kuwa kama ukurasa wa kwenye kitabu cha riwaya kwa namna nyingi, tatizo la msingi linabakia pale pale pasi na kujibiwa na Mrusi/Mwisraeli/Mreno huyu na kadi za kampuni yake.

Kulikoni mmiliki wa mali, kama hii klabu anaishi kwa kujificha na pasipo kuweka mambo wazi ili wadau wajue? Inakuwa kama mtu anayewasilisha ujumbe mithili ya alama za moshi na mara kadhaa kufukuza makocha?

Ni kwa vipi katika mchezo unaopendwa zaidi ulimwenguni tuliruhusu mtu mmoja – mtu yeyote – kuwa na mamlaka kiasi hiki na asiyegusika? Serikali za kidemokrasia huwajibika kwa waliozipigia kura, maofisa watendaji wakuu huwajibika kwa wanahisa. Je, Abramovich anawajibika kwa nani? Kwa Bodi ya Ligi Kuu? Kwa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA)? Kitu pekee tunachoweza kusema kwa uhakika mni kwamba huyu si Vladimir Putin. Hakik si Putin. Kabisa. Tunajua hayo kwa sababu mahakama ilisema hivyo, kwa hiyo lazima tuhitimishe kwamba mmiliki wa klabu wa sasa, kimsingi ni aina ya  mwasi, mwigizaji huru, hawajibiki kwa yeyote ila kwa dhamira yake ya kinadharia na mwito wa king’ora cha hamu yake mwenyewe.

Kuanzia kwa Mike Ashley pale Newcastle hadi kwa familia yaOyston pale Blackpool hadi kwa Glazers wa Manchester United, nenda kwa Mel Morris wa Derby, yeyote akiacha picha mbaya yaweza kuumiza sana washabiki wanaokutwa humo.

Kwa kiasi kikubwa, Abramovich amekuwa sawa na mwenye nyumba asiyeonwa na wapangaji wake, akiwachukua Chelsea waliokuwa chini kiasi 2003 hadi kuja kutwaa ubingwa, akaja kutumia pauni zaidi ya bilioni mbili kumsajili Nemanja Matic mara mbili. Licha ya timu kung’aa, bado amekuwa kimya, asitake kujibu maswali muhimu. Kulikoni soka? Kulikoni Chelsea? Ulianzaje kupata fedha  na ni kipi hasa anakitaka Uingereza?

Klabu kadhaa za Ligi Kuu ya England (EPL) zilitoka mikononi mwa wamiliki wa Kiingereza na kuchukuliwa na wageni wenye fedha nyingi na zinaendelea kutwaliwa. Na sasa soka inaanza kuamka. Washabiki wamekuwa na umoja hasa, katika nyakati mbalimbali, iwe timu zao zinafungwa au zinashinda.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0
Chelsea vs Liverpool

Uefa na Fifa wamechelewa: Urusi wamemaliza

Tanzania Sports

England