in ,

Platini ataka kura ya Qatar irudiwe

RAIS wa Shirikisho la Soka Ulaya (Uefa), Michel Platini amependekeza kurudiwa kwa kura juu ya uenyeji wa Kombe la Dunia 2022 kutokana na Qatar kupewa nafasi hiyo baada ya kughubikwa na tuhuma za rushwa.

Inadaiwa kwamba aliyekuwa Makamu wa Rais wa Fifa, Mohammed bin Hammam alitoa mamilioni ya dola kwa wajumbe wa mkutano huo ili waiunge mkono Qatar kuwa mwenyeji, ambapo walikubali na kutoa uenyeji majira ya kiangazi ambapo ni joto kali sana Mashariki ya Kati.

Tuhuma mpya na vielelezo vimetolewa wiki hii, ikiwa ni pamoja na mawasiliano ya Bin Hammam aliye kwenye Kamati ya Maandalizi ya Qatar kwa Kombe la Dunia 2022 na pia alitoa fedha taslimu kwa wajumbe.

Bin Hammam anadaiwa pia kutoa tiketi nyingi, suti, kuhudumia uenyeji wa Rais wa Shirikisho la Soka la Afrika (CAF), Issa Hayatou na kugharimia kesi ili kuzuia mjumbe ambaye angeweza kuiunga mkono Australia kuwa mwenyeji asipige kura, na kweli hakupiga.

Platini mwenyewe aliipigia kura Qatar lakini sasa anasema kwamba kutokana na uzito wa tuhuma na kama zitathibitishwa basi hakuna budi kura hiyo kurudiwa.
Wanasheria wameshaanza upelelezi kwa kutumia vielelezo husika juu ya tuhuma za rushwa, ambapo Fifa inaonekana kuzama kwenye kashfa kubwa.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Mtoto wa Pele jela miaka 33

England wana mtihani mkubwa