in , ,

Patrice Evra ajiunga Juventus

 

Nahodha Msaidizi wa Manchester United, Patrice Evra ameamua kuachana na timu hiyo na kujiunga na Juventus ya Italia.

Evra (33) ambaye ni beki wa kushoto aliyesaini mkataba mpya na Old Trafford majuzi, ameamua kujiunga na mabingwa hao wa Italia na atashiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya, kwani Man U hawashiriki chochote nje ya England msimu huu.

Mchezaji huyo anaondoka huku United wakiwa wameshamsajili beki chipukizi Luke Shaw kutoka Southampton kwa thamani ya pauni milioni 30.

Evra alikuwa mmoja wa wachezaji waliotishiwa kupigwa panga United lakini Ryan Giggs alipendekeza kwamba abaki pamoja na Rio Ferdinand. Hata hivyo mkataba wa Ferdinand haukuhuisha isipokuwa wa Evra tu.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Scolari aachia ngazi

‘Jaja’ wa Yanga huyu hapa