*Wapigwa 3-2 na JKT Ruvu, Azam sare
*Yanga wameung’ang’ania uongozi wa ligi

Wekundu wa Msimbazi – Simba wameshindwa kuchanua baada ya kushindwa kwata la maafande wa JKT Ruvu na kulala kwa mabao 3-2.

Katika mechiiliyopigwa Uwanja wa Taifa Jumapili hii, hadi nusu ya kwanza inamalizika Mnyama alikuwa akilia kwa mabao 2-0 yaliyopachikwa na Hussein Bunu na Emmanuel Swita.

Simba waliendelea kusuasua kipindi cha pili kwa kukubali bao la tatu, mfungaji akiwa tena Swita lakini Simba wakamrudi Amisi Tambwe aliyefunga mabao mawili, moja kwa penati na jingine akiunganisha majalo ya Amri Kiemba, lakini hayakutosha kuwapa ushindi wala sare.

Azam nao walishindwa kufurukuta vilivyo mbele ya maafande wa Prisons wa Mbeya, na kwenda nao sare ya 2-2.

Katika mechi ya Azam, Kipre Tchetche alizawadiwa kadi ya pili ya njano, kisha nyekundu katika dakika ya 58 na kuwafanya Azam kucheza pungufu.

Prisons walikuwa kwenye eneo la kushuka daraja, lakini kwa mechi tatu zilizopita wamebadilika na kushinda, na hata sare hapo Azam Complex ni pointi muhimu sana kwao.

Matokeo ya Jumapili hii yanamaanisha kwamba Yanga ambao ni mabingwa watetezi wanabaki kileleni kwa kuwa na pointi 38, Azam wakifuatia kwa pointi 37 huku Mbeya City wakiwa wa tatu kwa alama zao 35. Simba ni wa nne na mkusanyiko wao wa alama 32.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Arsenal karamu dhidi ya Sunderland

Liverpool kicheko, Spurs kilio