in , , ,

Oxlade-Chaberlain fiti Kombe la Dunia

Timu ya Taifa ya England imepata ahueni baada ya kubaini kwamba kiungo wao, Alex Oxlade-Chamberlain atakuwa fiti kucheza kwenye Kombe la Dunia nchini Brazil.

Ox, kama wanavyopenda kufupisha wenzake, aliumia goti kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Ecuador Jumatano iliyopita na palikuwa na wasiwasi kwamba mchezaji huyo wa Arsenal angeondolewa kwenye kikosi hicho.

Hata hivyo, Kocha Roy Hodgson amesema kwamba Ox atacheza bila wasiwasi, ikikumbukwa kwamba alikosa mechi kadhaa za Ligi Kuu ya England baada ya kuwa majeruhi. Katika mechi dhidi ya Ecuador matokeo yalikuwa 2-2 na Jumamosi hii walikwenda suluhu na Honduras.

Hii ilikuwa mechi ya mwisho ya maandalizi na sasa wanaelekea Brazil tayari kwa mashindano yatakayoanza rasmi Alhamisi hii. Nahodha Steven Gerrard alieleza kufurahishwa na uwapo wa Ox na kwamba kwenye mechi ya Jumamosi hapakuwa na majeruhi wapya licha ya makabiliano mabaya kutoka kwa wachezaji wa Honduras.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Frank Ribery nje Kombe la Dunia

Drogba kurudi Chelsea? Ni tetesi za usajili..