Mabingwa watetezi wa Afrika, Nigeria wameshindwa kufuzu kwa michuano ya Klabu Bingwa Afrika (AFCON), hivyo kutema ubingwa rasmi.

Nigeria imeshindwa kufuzu katika kundi ‘A’ ilikokuwa, hivyo itayasikia tu mashindano hayo yaliyopangwa kufanyika nchini Guinea ya Ikweta baada ya Morocco waliokuwa waandae kutofautiana na Shirikisho la Soka la Africa (Caf) juu ya masuala ya Ebola.

Katika mechi ya mwisho iliyofanyika Jumatano hii, Nigeria walibaniwa na Afrika Kusini mjini Uyo, wakaenda sare ya 2-2 hivyo kumaliza michuano nje ya nafasi mbili za juu kwa kundi lao.

Wangeweza kutarajia kupata nafasi ya timu bora zaidi katika nafasi za tatu lakini pia napo wameangukia pua, kwa sababu wana pointi nane tu. Afrika Kusini wamewakata maini Nigeria maana tayari walishafuzu kabla ya mechi hiyo, kwa mashindano yatakayofanyika kuanzia Januari 17 hadi Februari 8 mwakani.

nchi nyingine zilizofuzu kwa mashindano hayo makubwa Afrika ni Algeria, Burkina Faso, Cameroon, Cape Verde, Kongo Brazzaville, Kongo Kinshasa, Guinea ya Ikweta kwa nafasi ya wenyeji, Gabon, Ghana, Guinea, Ivory Coast, Mali, Senegal, Tunisia na Zambia waliofiwa na Rais Michael Satta majuzi.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Adele alikuwa sahihi kuwapuuza Bob Geldof na Band Aid

Arsenal nyumba ya njaa