in , ,

Mwali soka ya Afrika aanikwa

*AFCON iliyoanza Sudan 1957 yaenda Afrika Kusini

*Mataifa matatu yalianza kushiriki, leo fainali ni 16

Michuano ya 29 ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) inaanza Januari 19.

Kwa mara ya pili, Afrika Kusini itakuwa mwenyeji wa michezo hiyo itakayofanyika jijini Johannesburg, na miji mingine mikubwa ya Afrika Kusini.

Baada ya mwaka 1994 kuondokana na siasa za ubaguzi wa rangi zililoitenga, Afrika Kusini chini ya Rais Nelson Mandela iliandaa michezo hiyo mwaka 1996.

Hii ni michezo iliyoanza 1957, ikiandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF), ambapo wenyeji wa kwanza walikuwa Sudan, michuano ikafanyika Khartoum.

Enzi hizo ni nchi tatu tu zilishindana, nazo zilikuwa ni wenyeji Sudan, Misri na Ethiopia. Afrika Kusini waliokuwa wameshajumuishwa, walizuiwa ushiriki kutokana na siasa yao.

_58585843_sa_durb_stad_int_766gty

Haya ni mashindano ambayo hufanyika kila baada ya mwaka mmoja. Hata hivyo, mwaka jana yalifanyika Gabon na Guinea ya Ikweta na mwaka huu yanafanyika tena, lengo likiwa kubadili yasiangukie

mwaka wa Kombe la Dunia la FIFA linalofanyika kila baada ya miaka minne.

Michuano hii imetoka mbali, ambapo imepita kwenye awamu ya kukutanisha mataifa manne, sita kabla ya kuwa ya mataifa manane mwaka 1968 nchini Ethiopia.

Nchini Senegal mwaka 1992, michuano hii ilishirikisha mataifa 12, lakini tangu mwaka 1996 kule nchini Afrika Kusini, zinashiriki nchi 16.

_58347856_gab_v_mali_gtty

Hata hivyo, katika fainali hizo za 1996, licha ya timu 16 kufuzu, zilishiriki 15 kwa sababu mabingwa watetezi – Nigeria – walijitoa.

Walijitoa wakati wa mkesha wa ufunguzi, kwa sababu ya msigano wa kisiasa na kidiplomasia kati ya utawala wa kijeshi wa hayati Jenerali Sani Abacha na wa mzee Madiba.

Ni kwa bahati mbaya pia, michuano ya 27 iliyofanyika Angola mwaka 2010 ilishirikisha timu 15 badala ya 16, kwani Togo walijitoa siku chache kabla ya uzinduzi.

Walichukua hatua hiyo kutokana na kile walichoita kiwewe na mshituko baada ya msafara wa timu yao kushambuliwa, wawili wao kuuawa kwa risasi walipokuwa wakikatiza mpaka wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Angola.

Inaweza kusemwa kwamba historia ya michuano hii inazigusa zaidi timu tatu; Mafarao wa Misri, Black Stars wa Ghana na Simba Wasiofugika wa Cameroon.

Katika michuano 28 iliyopita, nchi tatu hizo zimefanikiwa kutwaa kombe mara 15 kati yao; Misri mara saba, kati ya hizo tatu mfululizo, wakiwa pia wameandaa mara nne.

Ghana wameshinda mara nne na wameandaa mara nne kadhalika, lakini ushindi na uandaaji havikufungamana.

Cameroon walikuwa wenyeji katika michuano ya nane tu, yaani mwaka 1972 na Simba wake wametwaa kombe mara nne.

Walitawazwa kuwa wafalme nchini Cote d’Ivoire mwaka 1984, ilipofanyika Moroco mwaka 1988, kule Ghana na Nigeria mwaka 2000 na nchini Mali mwaka 2002.

Mabingwa waliopita na waliokuwa wakipewa nafasi kubwa kutwaa tena, Cameroon, Misri na Cameroon walishangaza wengi kwa kushindwa kufika fainali za mwaka jana.

Ni ajabu bado, kwamba Mafarao wa Misri na Simba Wasiofugika wa Cameroon mwaka huu hawashiriki nchini Afrika Kusini, na wametolewa hatua za awali na nchi zilizodhaniwa kuwa ni vibonde.

—————————————————————————————————————-

Group Stages:

Sat 19 Jan      South Africa V Cape Verde  1600gmt Jo’burg

Sun 20 Jan     Ghana v DR Congo  1500gmt Port Elizabeth

Tues 22 Jan    Ivory Coast v Togo 1500 gmt Rustenburg

Thurs 24 Jan  Ghana v Mali 1500 gmt Port Elizabeth

Fri 25 Jan        Zambia v Nigeria 1500gmt

Mon 28 Jan     DRC v Mali 1700gmt Durban

Quarter Finals:

Sat 2 Feb          1500g Port Elizabeth

Sat 2 Feb          1830g Durban

Sun 3 Feb         1500g Rustenburg

Sun 3 Feb         1830g Nelspruit

 

Semi Finals

Wed 6 Feb       1500g Durban

Wed 6 Feb       1830g Nelspruit

 

Final

Sun 10 Feb      1800g Jo’burg

Enhanced by Zemanta

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Blatter: Boateng kafikisha ujumbe

Ronaldo hat-trick fires Real into Copa quarters