in , , ,

Frank Ribery nje Kombe la Dunia

 

 
Nyota wa Ufaransa, Frank Ribery ameondolewa
kwenye kikosi cha Timu ya Taifa ya Ufaransa kitakachoshiriki kwenye fainali za Kombe la Dunia.

Ribery (31) aliumia vibaya mgongo akiwa mazoezini na hivyo Kocha Didier Deschamps kukosa jingine la kufanya zaidi ya kumwondosha kikosini.

Kocha huyo wa Les Bleus amesema kwamba Ribery aliumia Ijumaa na hataweza kufanya mazoezi wala kucheza soka kwa majuma kadhaa.

Ribery alikuwa tegemeo kubwa, akiwa mahiri katika kuambaa na mpira kwenye wingi na kumimina majalo, ambapo angeshirikiana vyema na Olivier Giroud wa Arsenal.

Ribery anayechezea Bayern Munich amekipiga katika timu ya taifa mara 81 na kushiriki michuano ya Kombe la Dunia 2006 na 2010 na kuifungia timu hiyo mabao 16.

Mchezaji wa Lyon, Clement Grenier pia ameondolewa kwenye kikosi hicho baada ya kuumia hivyo mchezaji wa Southampton, Morgan Schneiderlin na Remy Cabella wa Montpellier wameitwa kuziba mapengo hayo.

Ribery amekuwa mchezaji bora wa Ufaransa kwa miaka mitatu na alichangia kwa kiasi kikubwa Ufaransa kufuzu kwa fainali hizi ambapo alifunga mabao matano.

Ribery mwaka jana alipigiwa kura na kushika nafasi ya tatu kwa uchezaji bora duniani, nyuma ya Cristiano Ronaldo wa Real Madrid na Lionel Messi wa Barcelona.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Wanachama Simba waenda FIFA….

Oxlade-Chaberlain fiti Kombe la Dunia