in , , ,

Nigeria wafuzu kwa mtoano

Nigeria wamekuwa taifa la kwanza Afrika kufuzu katika hatua ya makundi katika fainali za Kombe la Dunia nchini Brazil mwaka huu.

Nigeria wamefanikiwa kusonga mbele baada ya kutia kibindoni pointi nne kwa kushinda mechi moja, kwenda sare moja na kufungwa moja.

 

Walikuwa wakiwania nafasi ya pili nyuma ya Argentina na Iran ambao walikuwa na pointi moja.

Nigeria walifungwa na Argentina 3-2 Jumatano hii ambapo mabao mawili ya Argentina yalifungwa na Lionel Messi huku Ahmed Musa wa Nigeria akisawazisha moja baada ya jingine.

Lile la tatu na la ushindi kwa Argentina lilifungwa na mchezaji Rojo.

 

Stephen Keshi anakuwa kocha wa kwanza Mwafrika kuwavusha Waafrika hadi hatua ya mtoano, kwani timu nyingine zilizofuzu zimekuwa zikifundishwa na Wazungu, Wamarekani au Waasia.

Iran waliangukia pua baada ya kufungwa na Bosnia-Hercegovina katika mechi yao ya mwisho. Nigeria waliwafunga Bosnia na kwenda suluhu na Iran katika mechi zake za awali.

 

Argentina wameshinda mechi zao zote tatu na katika hatua ya mtoano Nigeria watachuana na Ufaransa ambao wameshinda mechi mbili na kwenda sare moja.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Suarez kikaangoni Fifa

Ghana wawafukuza Boateng, Muntari