in , , ,

NI TETESI ZA USAJILI

Sterling : anaumiza vichwa vya Arsenal na Man City....

TETESI ZA USAJILI

 

Man City kuwabomoa Liverpool?

 

Mabingwa watetezi wa England, Manchester City wanataka kusajili wachezaji watatu kutoka Liverpool.

 

Matajiri hao wanataka kumsajili kiungo mchezeshaji, Philippe Coutinho (22),mshambuliaji Raheem Sterling (20) aliyekataa mkataba mpya Anfield na kiungo Jordan Henderson (24) anayesuasua kupokea dili jipya hapo.

 

Pamoja na kwamba Liverpool wangependa kubakiza wachezaji hao wote, wanakosa nguvu ya fedha kuchuana na klabu nyingine kubwa za England.

Jack

 

Chelsea, Manchester United na Arsenal wanawafuatilia kwa karibu beki wa kulia wa Southampton, Nathaniel Clyne (24) na kiungo wao, Morgan Schneiderlin (25).

 

Mlinzi wa Valencia, Andres Gomes (21) amekanusha madai kwamba anakaribia kujiunga na Chelsea.

 

Kwingineko, Barcelona wamesema milango ipo wazi kwa ajili ya kujadiliana na kiungo wao mkongwe, Xavi ilia pate mkataba mpya, lakini Xavi (35) anadaiwa amepanga kujiunga na klabu ya Al Sadd ya Qatar.

 

Kocha anayewasaidia Sunderland kuepuka kushuka daraja, Dick Advocaat atapewa mkataba wa mwaka mmoja iwapo atafanikisha kazi hiyo.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Gabon mwenyeji AFCON 2017

Walcott Liverpool, Sterling Arsenal?