in , ,

NI Simba na Yanga leo…..

 

Yanga nao wanasema haiwezekani washindwe kuifunga timu ambayo imepata kibahati nafasi ya tatu. Kwa ufupi timu zote zinatumia neno hili ‘haiwezekani”.

 

Maskani ya Simba na Yanga ni Dar es Salaam, lakini zilikimbilia Zanzibar. Simba ilibana Unguja Yanga ikapanda mpaka Pemba.

 

Zimejigamba na kujisifu vya kutosha lakini leo Jumamosi ni ukweli utajulikana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

 

Simba haina nafasi ya kushiriki michuano mikubwa mwakani, lakini ina uhakika wa Sh. 25 milioni kama zawadi ya mshindi wa tatu wa ligi na inaikabili Yanga leo Jumamosi jioni kwenye Uwanja wa Taifa kulinda heshima na kukamilisha msimu.

 

Yanga tayari ni mabingwa na wana uhakika wa Sh.70 milioni za mshindi wa kwanza.

 

Simba na Yanga zilirejea jana Ijumaa Dar es Salaam zikitokea Zanzibar zilipokuwa zimepiga kambi wakati Yanga ilikuwa Pemba, watani wao Simba walikuwa Unguja.

 

Kocha wa Simba, Patrick Liewig amesisitiza kwamba timu yake ina morali na wachezaji wake vijana wametulia kisaikolojia tayari kuikabili Yanga ambayo bosi wake Ernest Brandts amesema watafanya vitendo uwanjani.

DSC03050

 

Simba imekuwa ikiwatumia yosso wake katika mechi za karibuni, lakini katika mchezo wa leo Jumamosi itaweka mchanganyiko zaidi na kuwatumia wazoefu wengi.

 

Itaingiza kikosi kitakachoundwa na mabeki; Nasor Said ‘Chollo’, Haruna Shamte, Mussa Mude na Shomari Kapombe kumlinda Abeil Dhaira.

 

Katika kiungo watacheza; Amri Kiemba, Mwinyi Kazimoto,William Lucian na Haruna Chanongo,wakati kwenye ushambuliaji watasimama Mrisho Ngassa na Felix Sunzu.

 

Katika benchi lao watajaza vijana wengi kama Christopher Edward, Ramadhani Singano, Miraji Adam, Abdallah Seseme, na Hassan Khatib.

 

Enhanced by Zemanta

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Beckham: Miaka 20 safi ya soka

Yanga wachinja mnyama Taifa