in , ,

Mikel Arteta, na Arsenal watembee kifua mbele

MANCHESTER CITY ni mabingwa wa EPL msimu huu. Pongezi nyingi kwao. Lakini

macho,akili na hisia zangu zimeona kitu kingine kutoka kwa wapinzani wao, Arsenal. Ni ukweli

usipoingika kuwa Arsenal walikuwa na kila sababu ya kuchukua ubingwa wa Ligi Kuu England

msimu huu, lakini ajali ya mechi kadhaa kupata matokeo mabaya yaliwanyima ubingwa wa Ligi

Kuu.

Kwangu mimi Arsenal ni mabingwa ambao wanatakiwa kutembea kifua mbele. Timu hii ilianza

Ligi ikiwa haipewi nafasi ya kuingia hata nne bora. Wasiwasi dhidi ya Arsenal ulikuwa mkubwa

kwa watu, huku wapinzani wake wakiipuuza kwa kuamini hawawezi kupata hata nafasi ya

kuwakilisha Europa Lague au Conference League. Arsenal ni timu ambayo imeonekana kama

vile iliyumba tangu kuondoka kwa gwiji wake Arsene Wenger.

Pengine Arsene Wenger yungali katika viunga vya Arsenal. Ni timu ambayo inaoongozwa na

wachezaji wa zamani wa Arsene Wenger ndio waliokuwa na imani kuwa Arsenal inaweza

kuleta kitu cha kipeke EPL. Msimu unamalizika, Arsenal hii ikiwa chini ya kocha wake Mikel

Arteta, na Mkurugenzi wa Michezo,

Tanzania Sports

Edu Gaspar wameleta kitu kizuri kwa Arsenal ambacho kitawafanya washabiki wake wafurahie

licha ya kuukosa ubingwa dakika za lala salama. Arteta ni raia wa Hispania, ameleta ufundi na

utamaduni wa Kihispaniola.

Edu Gaspar ni raia wa Brazil, ambaye ametoka taifa kubwa na lenye sifa nyingi katika

ulimwengu wa soka. Brazil ndio mabingwa wa dunia wenye mataji matano kuliko nchi nyingine

yoyote. Edu Gaspar ameleta utamaduni wa Kibrazil na amejifunza ule wa Kishipania ambako

aliichezea klabu ya Valencia.

Wawili hawa ndio wanatakiwa kupendwa, kuengwa engwa na mashabiki wa Arsenal ambao

walifanywa waamini kuwa timu yao ilikuwa kwenye mbio za ubingwa. Wakati wanawasajili

Alexandre Zinchenko, Tossard,Gabreil Jesus, na vijana wengine hakuna aliyedhania kuwa

Arsenal ingekuja kutikisa vigogo EPL.

Chini ya Arteta na Edu maelfu ya wanamichezo duniani wameona kitu walichokileta viongozi

hao wawili na wasaidizi wao. Licha ya wastani wa umri wa wachezaji wao kuwa chini ya miaka

25, Arsenal hii imepiga hatua kubwa na kurejesha tabasamu kwa mashabiki.

Ubingwa wa Arsenal umekuja katika kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Katika

kipindi cha Arsene Wenger, ilijulikana kuwa Arsenal haikuwa na shida katika kupigania nafasi

nne za kuwakilisha mashindano ya Ulaya. Ilikuwa hata vita iweje, lakini Wenger angeshinda

kiulaini.

Hata hivyo Arsenal ilipotea kwa muda kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa, jitihada zao

ziliishia kwenye Europa League. Hapo ndipo utaona Edu na Arteta watakuwa wenye wingi wa

furaha kuirudisha timu kwenye mashindano ambayo wao wakiwa wachezaji walikuwa

wamezoea na kuyacheza mara nyingi.

Arsenal ilikuwa mali ya Ligi ya Mabingwa, na Edu na Arteta wameipa kile inachostahili.

Naamini kati ya vipaumbele vikubwa vilivyokuwa mezani mwa Arteta na Edu, kikubwa

kilikuwa kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya. Wawili hawa wamefanya kazi kubwa ambayo

imevuka matarajio yao kwani Arsenal ilikuwa mshindani mkali wa taji la EPL dhidi ya

Manchester City.

Nina uhakika huenda Pep Guardiola na timu yao ya uongozi hawatakuwa tayari kuwauzia

mchezaji mwingine Arsenal. Msimu huu waliuza Zinchenko na Gabriel Jesus kwenda Arsenal,

ambao walikuwa chachu ya kuimarisha kikosi cha Arteta na Edu.

Hii ina maana Edu alileta kipaji cha Kibrazil (utamaduni wa kwao) na akaongeza ufundi wa

Zinchenko toka Ukraine. Bila kujali mifumo iliyotumika katika mbio za EPL, Arsenal

wanapaswa kufurahia matokeo waliyopata; wamekosa ubingwa lakini wamefuzu Ligi ya

Mabingwa Ulaya.

Kama kuna jambo ambalo Edu na Arteta wanapaswa kulifanya kwa sasa ni kuimarisha kikosi

chao katika maeneo haya; beki wa kati mmoja, kiungo mkabaji mmoja,mshambuliaji mmoja na

beki wa kushoto mmoja.

Lengo ni kuimarisha ubora wa idara hizo pamoja na kuipa machaguo ya kutosha inapoelekea

kwenye Ligi ya Mabingwa. Safu ya ushambuliaji inahitaji mshambuliaji mwingine ambaye

atakuwa mpango wa pili wa Gabreil Jesus, hii ina maana Eddie Nketiah bado anatakiwa

kuimarika na kwenye mashindano ya Ulaya muda huo haupo.

Ni wazi Arsenal lazima iingie sokoni katika eneo la ushambuliaji mwenye uwezo wa kufunga

mabao zaidi ya 20 kwa msimu. Vilevile eneo la beki wa kushoto Zinchenko anaonekana pia

kufaa kucheza kiungo au winga wa kushoto, kwahiyo katika mfumo wa kuimarisha ulinzi

anahitajika beki wa kushoto kumpa nafasi kocha kuwa na machaguo mazuri.

Eneo la kiungo mkabaji, Jorginho na Thomas Partey wanahitaji mshindani mwingine licha ya

umri wao kupaa zaidi. Ni eneo ambalo limewafanya Arsenal kupoteana pale wanaodhibitiwa

kwenye kiungo mkabaji.

Idara nyingine ni beki wa kati, ni eneo ambalo Edu na Mikel Arteta wanapaswa kufanyia kazi

kama njia ya kuboresha kikosi chao. Ifahamike Ligi ya Mabingwa hukutanisha timu zenye

viwango bora zaidi kuanzia mchezaji mmoja mmoja hadi makocha. Ni muhimu Arsenal kuwa

tayari katika ushindani huu. Vilevile, mashabiki waelewe ikiwa hawakutegemea kuona ushindani

wa timu yao kwenye EPL, ni kwa kiasi gani wanaweza kupunguza imani kwa Arsenal kufanya

vizuri kwenye Ligi ya Mabingwa?

Ni lazima wawe tayari kuinga mkono timu hii na viongozi wawo hawa hawa. Washabiki

hawapaswi kuondoka uwanjani pale juhudi za wachezaji wao zinapokwama. Washabiki

wapambane kwa kuiunga mkono timu hadi dakika za mwisho.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

72 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0
Tanzania Sports

Dakika za lala salama kuwapasua vigogo EPL

Tanzania Sports

Yanga wameloweshwa nyumbani, kung’ara ugenini?