in , ,

MIKAKATI YA KUENDELEZA MPIRA WA MIGUU KWA WANAWAKE

*Ni hatua muhimu katika kukuza soka la kinamama

Utangulizi:

Awali ya yote napenda kuchukua nafasi hii kwa niaba ya kamati ya utendaji ya TWFA kuwashukuru wajumbe wa mkutano mkuu kwa kutupa ridhaa ya kuongoza chama kwa kipindi cha miaka minne.

 

Pia napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru wadau wote wa mpira wa miguu kwa kutuwezesha kufika hapa tulipo. Napenda niwashukuru wadau wote kwa ujumla wao na pia kuishukuru serikali kwa namna ya pekee zaidi kwa mchango wake ,na mashirika na makampuni ambayo yamekuwa karibu sana nasi NMB, SERENGETI, NSSF, PPF, na Bakheresa Group of Companies.

 

Tunaamini kabisa kuwa vyombo vya habari ni washirika wetu wakubwa katika kuendeleza mpira wa miguu wanawake. Napenda kuvishukuru vyombo vyote vya habari hapa nchini na hata vile vya nje vilivyoweza kutoa nafasi katika ujenzi wa mpira wa miguu wanawake.

 

 Maendeleo ya mpira

 Kutekeleza na kuendeleza mpango wa grassroot.

 

Kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira wa miguu Tanzania,Chama cha Mpira  wa Miguu wanawake  na vyama vya mikoa na wadau mbalimbali  tutaendelea kuendeleza mradi wa mpira wa miguu kwa watoto wa kike na wa kiume Grassroot programme.(umri wa miaka 06-12).kwa mwaka 2013 mradi huu utatekelezwa katika mikoa  mitano (5) mikoa hiyo ni  Tanga,Pwani.Mwanza,Mtwara na Lindi. Mradi huu unaendeshwa kupitia shule za msingi.Kwa mwaka 2012 Mradi huu umeendeshwa katika mkoa wa Dar es Salaam na  watoto wapatao 8766 (wasichana 4909 na wavulana 3857 ) na walimu 26 wameshirikishwa.

 

Mafunzo ,semina na makongamano

Kwa mwaka 2013 tunatengemea kuendesha mafunzo mbalimbali katika nyanja kuu nne za maendeleo ya mpira wa miguu yaani Utawala na uongozi,Ualimu(Ukocha)  Uamuzi na utabibu katika mpira wa miguu .Katika mwaka mwaka 2013 mafunzo yatafanyika zaidi katika nyanja ya uongozi ili kuwajengea stadi za uongozi viongozi wengi ambao wameingia madarakani katika chaguzi zilizofanyika kwa mwaka 2012/2013.Mafunzo ya utawala na uongozi yatafanyika katika mikoa nane:Dar es Salaam,Pwani,Morogoro,Mwanza,Musoma,Shinyanga,Kilimanjaro na Tanga.Katika mafunzo hayo baadhi ya washiriki watateuliwa kutokana na uwezo wao kwa kuzingatia vigezo vitakavyowekwa na watahudhuria semina itakayo andaliwa kwa kushirikiana na shirikisho la mpira wa miguu Tanzania.

 

Mafunzo kwa walimu katika ngazi mbalimbali na uratibu wa utekelezaji wa mafunzo yaliyofanyika yatapewa kipau mbele.

 

Mafunzo kwa waamuzi yatalenga zaidi kuibua vipaji vya watoto wa kike walioko mashuleni na wachezaji wanaomaliza/waliomaliza muda wao.Mafunzo yatafanyika kwa awamu mbili katika mkoa wa Dar es Salaam.

 

Madaktari  wa michezo  ni muhimu sana katika maendeleo ya mpira na afya za wachezaji kwa kushirikiana na vyombo husika mafunzo kwa mwaka 2013 yatafanyika kwa awamu mbili na yatafanyika katika mkoa wa Dar es Salaam.

Wanahabari wenye uweledi katika mpira wa miguu wa wanawake ni chachu ya maendeleo ya mpira huo.Nafasi ya wanahabari ni kubwa katika kuendeleza mpira wa miguu ili kuwajengea ujuzi zaidi kutakuwa na mafunzo kwa wanahabari yatakayofanyika Dar es Salaam.

 

Uongozi na utawala bora

Maendeleo ya mpira wa miguu kwa wanawake yanahitaji viongozi bora na waliopewa ridhaa na vyombo husika.Chaguzi zimefanyika katika  mikoa 16 kati 25  ya mikoa ya Tanzania Bara. Pia tunahimiza mikoa ambayo haijafanya uchaguzi ifanye chaguzi mapema.  Mikoa hiyo ni: Dar es salaam, Mwanza, Kilimanjaro, Rukwa, Arusha, Geita, Simiyu, Njombe, Katavi na Mbeya.

 

Katika chaguzi hizo kuna baadhi nafasi zote hazikujazwa ni matumaini yetu kuwa  zitajazwa katika mikutano ijayo ya vyama husika.

Pia nichukue nafasi hii kuwahamasisha kina mama wengi wenye sifa kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali katika vyama vya mikoa na taifa pale uchaguzi utakapoitishwa.

 

Mashindano

Mashindano mbalimbali ndio moyo wa mpira wa miguu bila mashindano  hakuna anayeweza kutambua  ubora na kiwango chakena pia ni kipimo cha maendeleo.

Kutakuwa na mashindano mbalimbali katika ngazi ya  mikoa,taifa na kimataifa.

Mashindano hayo pia yatahusisha shule za msingi na sekondari  na vyuo mbalimbali.Kwa kushirikiana na vyombo husika kutakuwa na ufuatiliaji wa karibu wa michezo ya UMISSETA toka ngazi ya mkoa hadi Taifa na kuwa na mpango endelevu wa kuwaendeleza wale wenye vipaji ambao wamechaguliwa /wanaweza kuchaguliwa kwenye timu za taifa.

 

Ligi itachezwa katika ngazi za mikoa na baadaye kuunda kombaini ya mkoa itakayoshiriki mashindano ya taifa.

 

Kwa mwaka 2013 tunatengemea mikoa kuchezesha ligi isiyopungua timu tano kwa mikoa 15 itakuwa na timu  10 na timu itaruhusiwa kusajili wachezaji 25 kwa mwaka 2013 tunatengemea watoto/wasichana  3750 kushiriki katika mpira wa miguu. Idadi hii ukizidisha mara nne unapata jumla ya wachezaji 15,000.Endapo tutakuwa na benki ya wachezaji hawa tutaweza kuunda timu bora za umri tofauti na zenye kiwango cha juu.

 

Pia mikoa inahimizwa kuanzisha mashindano mbalimbali yatakayoamsha ari kwa watoto wa kike na wasichana kushiriki katika mpira wa miguu.

 

Uratibu wa mikoa

Wajumbe wa kamati ya utendaji pamoja na  majukumu yao kama wajumbe watakuwa na jukumu la kuratibu shughuli za  maendeleo ya mpira wa miguu katika mikoa:Uratibu huo utakuwa kama ifuatavyo:

Rose Kissiwa Makamu Mwenyekiti Tabora, Dodoma, Rukwa, Kigoma, Pwani
Amina Karuma Katibu Lindi, Mtwara, Iringa, Njombe, Ruvuma
Zena Chande Mjumbe Dar es Salaam, Morogoro, Katavi, Shinyanga, Mbeya
Triphonia Temba Mjumbe Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Singida
Sophia Charles Mjumbe Mara, Kagera, Simiyu, Geita, Mwanza

Kwa mujibu wa katiba ya TWFA  ibara ya 37  inatoa nafasi kwa kamati ya utendaji kuunda kamati ndogo za kuendeleza mpira wa miguu wanawake kamati hizo ni kamati ya Fedha na mipango,kamati ya Ufundi,kamati ya ngingine itakayoonekana inafaa.Kamati ya utendaji kwa pamoja ilikubaliana kuunda kamati ya habari na masoko.

Kamati ya Fedha na Mipango

1.     Rose Kissiwa       – Mwenyekiti

2.     Evans Aveva

3.     Sophia Tigalyoma

4.     Sophia Mukama

5.     Asha Baraka

Kamati ya Ufundi

1.     Tryphonia Temba – Mwenyekiti

2.     Florence Ambonisye

3.     Miraji Fundi

4.     Dr. Leonia Kaijage

5.     Furaha Francis

6.     Richard Muhotoli

Kamati ya Habari na Masoko

1.     Zena Chande – Mwenyekiti

2.     Beatrice Mgaya

3.     Mohamed Mkangara

4.     Florian Kaijage

5.     Somoe Ng’itu

 

Masoko na Habari

Mpira wa miguu wanawake hauna udhamini na pia vyanzo rasmi vya kupata mapato.Kwa kupitia kamati ya habari na masoko ,tunaamini kutakuwa na mikakakti mbalimbali ya kuelimisha ,kuhamasisha wadau na watanzania wote kuwiwa na kujitoa kuendeleza mpira wa miguu .

 

 

Asanteni

Lina P.Kessy

Mwenyekiti Chama cha Mpira wa miguu wanawake 

Enhanced by Zemanta

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Arsenal kuwabomoa Swansea

FA Cup….