in , ,

Man U wanachekelea

*Jose Mourinho ametwaa kombe la kwanza na klabu yake mpya ya Manchester United*

Wakiwa bado katika nafasi yao waliyozoea ya sita kwenye msimamo wa
Ligi Kuu ya England (EPL), Man U walitwaa Kombe la Ligi – EFL baada ya
kuwafunga Southampton 3-2.
Alikuwa mshambuliaji hatari aliyesajiliwa bila ada, Zlatan
Ibrahimovic, 35, aliyefunga bao la ushindi dakika tatu tu kabla ya
muda wa mchezo kumalizika.
Saints walikuwa makini kwenye Uwanja wa Taifa – Wembley, lakini
walizidiwa dakika za mwisho na kuruhusu bao hilo. Kwa muda mwingi wa
mchezo walikuwa wazuri kuliko Man U.
Walivunjwa moyo pia kukataliwa bao la Manolo Gabbiadini kwa madai ya
mchezaji huyo kuotea, kana kwamba hiyo haitoshi Ibrahimovic
akawamaliza, akifunga bao lake la 26 kwa msimu huu katika mashindano
yote.
United walishafunga mabao mawili ya kuongoza kupitia kwa Ibrahimovic
na Jesse Lingard, lakini Saints wakapambana na kusawazisha kupitia kwa
Gabbiadini, bao moja kila kipindi.
Mourinho alionekana kutofurahia ufanisi wa timu yake kwenye fainali
hii, na atawakazania wachezaji wake zaidi kuongeza umakini kwenye
kazi. Hata hivyo, atafurahi kuweka historia kutwaa kombe na klabu hii
kubwa.
Amekuwa akililenga kombe hili, kwani mwaka 2005 aliwafunga Liverpool
akiwa na Chelsea uwanani japo na 2015 kadhalika, akiwafunga Tottenham
Hotspur.
United watakuwa Old Trafford kwao Jumamosi hii kuwakabili Bournemouth
kwenye EPL mchana wakati Saints watakuwa na kazi ya kupambana na
Watford.

==mwisho==

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

NILICHOKIONA KWENYE MECHI YA SIMBA NA YANGA JANA.

Tanzania Sports

RUVU Shooting 0-2 Yanga : Mambo manne tuliyo jifunza