in , , ,

Man U wakwama Sunderland

Manchester United wameshindwa kutoka kwenye mtanziko wa kuanza vibaya ligi kuu.

Vijana wa Louis van Gaal wameambulia sare ya 1-1 nyumbani kwa Sunderland, na kumfanya Mdachi huyo aendelee kusubiri ushindi wake wa kwanza.

Juan Mata alitoa matumaini kwa kufunga bao dakika ya 17 lakini likafutwa na Jack Rodwell dakika 15 kabla ya mapumziko. Kadiri muda ulivyokwenda ufanisi wa Mata kwenye wingi ulipungua kwa kuzidiwa maarifa na Lee Cattermore na pia Nahodha Wayne Rooney hakufurukuta.                           

Mbaya zaidi, Ashley Young akishambulia ndani ya eneo la penati alijirusha, wakadai penati lakini akaishia kupewa kadi ya njano.  

Van Gaal na msaidizi wake, Ryan Giggs walizama katika majadiliano kuubadili mchezo ila itabidi waridhike na pointi moja waliyopata kwani walikuwa kikawaida sana.  Itabidi Man u wajitahidi kusajili wachezaji wengine wazuri.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Di Maria: Man United kutoa £75m?

Algeria wasitisha ligi